Zaburi 98:1-9
-
Yehova ni Mwokozi na Muamuzi mwenye haki
-
Wokovu wa Yehova unajulishwa (2, 3)
-
Muziki.
98 Mumuimbie Yehova wimbo mupya,+Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+
Mukono wake wa kuume, mukono wake mutakatifu, umeleta wokovu.*+
2 Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+Amefunua haki yake mbele ya mataifa.+
3 Amekumbuka upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake kuelekea nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeona wokovu* wa Mungu wetu.+
4 Mumupigie Yehova vigelegele vya ushindi, dunia yote.
Muchangamuke na mupige vigelegele vya shangwe na kuimba sifa.*+
5 Mumuimbie Yehova sifa* kwa kinubi,Kwa kinubi na wimbo mutamu.
6 Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu,+Mupige vigelegele vya ushindi mbele ya Mufalme, Yehova.
7 Acha bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza,Dunia* na wale wenye kukaa ndani yake.
8 Mito ipige mikono;Milima ipige pamoja vigelegele vya shangwe+
9 Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja* kuhukumu dunia.
Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu*+Na vikundi vya watu kwa haki.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “umemuletea ushindi.”
^ Ao “ushindi.”
^ Ao “kupiga muziki.”
^ Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
^ Ao “Inchi yenye kuzaa.”
^ Ao “amekuja.”
^ Ao “inchi yenye kuzaa.”