Zaburi 98:1-9

  • Yehova ni Mwokozi na Muamuzi mwenye haki

    • Wokovu wa Yehova unajulishwa (2, 3)

Muziki. 98  Mumuimbie Yehova wimbo mupya,+ Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+ Mukono wake wa kuume, mukono wake mutakatifu, umeleta wokovu.*+   Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+ Amefunua haki yake mbele ya mataifa.+   Amekumbuka upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake kuelekea nyumba ya Israeli.+ Miisho yote ya dunia imeona wokovu* wa Mungu wetu.+   Mumupigie Yehova vigelegele vya ushindi, dunia yote. Muchangamuke na mupige vigelegele vya shangwe na kuimba sifa.*+   Mumuimbie Yehova sifa* kwa kinubi, Kwa kinubi na wimbo mutamu.   Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu,+ Mupige vigelegele vya ushindi mbele ya Mufalme, Yehova.   Acha bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza, Dunia* na wale wenye kukaa ndani yake.   Mito ipige mikono; Milima ipige pamoja vigelegele vya shangwe+   Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja* kuhukumu dunia. Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu*+ Na vikundi vya watu kwa haki.+

Maelezo ya Chini

Ao “umemuletea ushindi.”
Ao “ushindi.”
Ao “kupiga muziki.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Ao “Inchi yenye kuzaa.”
Ao “amekuja.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”