Zaburi 98:1-9

  • Yehova ni Mwokozi na Muamuzi mwenye haki

    • Wokovu wa Yehova unajulishwa (2, 3)

Muziki. 98  Mumuimbie Yehova wimbo mupya,+Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+ Mukono wake wa kuume, mukono wake mutakatifu, umeleta wokovu.*+  2  Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+Amefunua haki yake mbele ya mataifa.+  3  Amekumbuka upendo wake mushikamanifu na uaminifu wake kuelekea nyumba ya Israeli.+ Miisho yote ya dunia imeona wokovu* wa Mungu wetu.+  4  Mumupigie Yehova vigelegele vya ushindi, dunia yote. Muchangamuke na mupige vigelegele vya shangwe na kuimba sifa.*+  5  Mumuimbie Yehova sifa* kwa kinubi,Kwa kinubi na wimbo mutamu.  6  Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu,+Mupige vigelegele vya ushindi mbele ya Mufalme, Yehova.  7  Acha bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza,Dunia* na wale wenye kukaa ndani yake.  8  Mito ipige mikono;Milima ipige pamoja vigelegele vya shangwe+  9  Mbele ya Yehova, kwa maana anakuja* kuhukumu dunia. Atahukumu kwa haki dunia yenye kuikaliwa na watu*+Na vikundi vya watu kwa haki.+

Maelezo ya Chini

Ao “umemuletea ushindi.”
Ao “ushindi.”
Ao “kupiga muziki.”
Ao “Mumupigie Yehova muziki.”
Ao “Inchi yenye kuzaa.”
Ao “amekuja.”
Ao “inchi yenye kuzaa.”