Zaburi 73:1-28
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale wenye kuwa safi katika moyo.+
2 Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kutoka katika njia;Hatua zangu zilikuwa karibu kutereza.+
3 Kwa maana nilisikilia wivu wenye kiburi*Wakati nilikuwa ninaona amani ya waovu.+
4 Kwa maana hawana maumivu wakati wanakufa;Miili yao iko na afya ya muzuri.*+
5 Hawasumbuke kama wanadamu wengine,+Wala hawateseke kama watu wengine.+
6 Kwa hiyo, kiburi ni mukufu wao wa shingo;+Jeuri inawafunika kama nguo.
7 Mafanikio* yao yanafanya macho yao yavimbe;Wamezidi mawazo ya moyo.
8 Wanachekelea na kusema mambo maovu.+
Kwa kiburi, wanaogopesha ili kukandamiza.+
9 Wanaongea kama vile wako juu kama mbingu,Na ndimi zao zinatembea huku na huku zikijisifu katika dunia.
10 Kwa hiyo watu wake wanawaendea,Na wanakunywa kutokana na maji yao mengi.
11 Wanasema: “Mungu anajua namna gani?+
Je, Mwenye Kuwa Juu Zaidi iko* kabisa na ujuzi?”
12 Ndiyo, hiyo ndiyo hali ya waovu, wenye sikuzote wanafurahia maisha.+
Wanaendelea kuongeza mali zao.+
13 Hakika nimesafisha moyo wangu bureNa kunawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia.+
14 Na nilisumbuka muchana wote;+Nilipewa azabu kila asubui.+
15 Lakini kama ningesema mambo hayo,Ningekuwa nimesaliti watu wako.*
16 Wakati nilijaribu kuelewa jambo hilo,Lilinisumbua
17 Mupaka wakati niliingia katika patakatifu pakubwa pa Mungu,Na nikatambua wakati wao wenye kuja.
18 Hakika unawatia kwenye udongo wenye kutereza.+
Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+
19 Wanaharibiwa bila kutazamia kabisa!+
Wanamalizika kwa kushitukia kabisa wakati wanafikia mwisho wao mubaya sana!
20 Kama ndoto wakati wa kuamuka, Ee Yehova,Wakati utasimama, utatupilia mbali* sanamu yao.
21 Lakini moyo wangu ulikuwa muchungu,+Na ndani kabisa* nilisikia maumivu makali.
22 Sikukuwa na akili na nilikosa uelewaji;Nilikuwa kama munyama mwenye hana akili mbele yako.
23 Lakini sasa niko pamoja na wewe sikuzote;Umeshika mukono wangu wa kuume.+
24 Unaniongoza kupitia shauri lako,+Na kisha utaniongoza kwenye utukufu.+
25 Ni nani mwenye niko naye kule mbinguni?
Na sitamani kitu chochote katika dunia isipokuwa wewe tu.+
26 Mwili wangu na moyo wangu unaweza kuchoka,Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+
27 Kwa kweli, wale wenye kujitenga mbali na wewe wataangamia.
Utaharibu* kila mutu mwenye anakuacha kwa sababu ya upotovu.*+
28 Lakini mimi, kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu.+
Nimemufanya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova kuwa kimbilio langu,Ili nitangaze kazi zako zote.+

