Zaburi 73:1-28

  • Mutu mwenye kumuogopa Mungu anarudiwa na ufahamu wa kiroho

    • “Miguu yangu ilikuwa karibu kutoka katika njia” (2)

    • “Nilisumbuka muchana wote” (14)

    • ‘Mupaka wakati niliingia katika patakatifu pa Mungu’ (17)

    • Waovu wako kwenye udongo wenye kutereza (18)

    • Kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri (28)

Muziki wa Asafu.+ 73  Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale wenye kuwa safi katika moyo.+  2  Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kutoka katika njia;Hatua zangu zilikuwa karibu kutereza.+  3  Kwa maana nilisikilia wivu wenye kiburi*Wakati nilikuwa ninaona amani ya waovu.+  4  Kwa maana hawana maumivu wakati wanakufa;Miili yao iko na afya ya muzuri.*+  5  Hawasumbuke kama wanadamu wengine,+Wala hawateseke kama watu wengine.+  6  Kwa hiyo, kiburi ni mukufu wao wa shingo;+Jeuri inawafunika kama nguo.  7  Mafanikio* yao yanafanya macho yao yavimbe;Wamezidi mawazo ya moyo.  8  Wanachekelea na kusema mambo maovu.+ Kwa kiburi, wanaogopesha ili kukandamiza.+  9  Wanaongea kama vile wako juu kama mbingu,Na ndimi zao zinatembea huku na huku zikijisifu katika dunia. 10  Kwa hiyo watu wake wanawaendea,Na wanakunywa kutokana na maji yao mengi. 11  Wanasema: “Mungu anajua namna gani?+ Je, Mwenye Kuwa Juu Zaidi iko* kabisa na ujuzi?” 12  Ndiyo, hiyo ndiyo hali ya waovu, wenye sikuzote wanafurahia maisha.+ Wanaendelea kuongeza mali zao.+ 13  Hakika nimesafisha moyo wangu bureNa kunawa mikono yangu katika kukosa kuwa na hatia.+ 14  Na nilisumbuka muchana wote;+Nilipewa azabu kila asubui.+ 15  Lakini kama ningesema mambo hayo,Ningekuwa nimesaliti watu wako.* 16  Wakati nilijaribu kuelewa jambo hilo,Lilinisumbua 17  Mupaka wakati niliingia katika patakatifu pakubwa pa Mungu,Na nikatambua wakati wao wenye kuja. 18  Hakika unawatia kwenye udongo wenye kutereza.+ Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+ 19  Wanaharibiwa bila kutazamia kabisa!+ Wanamalizika kwa kushitukia kabisa wakati wanafikia mwisho wao mubaya sana! 20  Kama ndoto wakati wa kuamuka, Ee Yehova,Wakati utasimama, utatupilia mbali* sanamu yao. 21  Lakini moyo wangu ulikuwa muchungu,+Na ndani kabisa* nilisikia maumivu makali. 22  Sikukuwa na akili na nilikosa uelewaji;Nilikuwa kama munyama mwenye hana akili mbele yako. 23  Lakini sasa niko pamoja na wewe sikuzote;Umeshika mukono wangu wa kuume.+ 24  Unaniongoza kupitia shauri lako,+Na kisha utaniongoza kwenye utukufu.+ 25  Ni nani mwenye niko naye kule mbinguni? Na sitamani kitu chochote katika dunia isipokuwa wewe tu.+ 26  Mwili wangu na moyo wangu unaweza kuchoka,Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+ 27  Kwa kweli, wale wenye kujitenga mbali na wewe wataangamia. Utaharibu* kila mutu mwenye anakuacha kwa sababu ya upotovu.*+ 28  Lakini mimi, kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu.+ Nimemufanya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova kuwa kimbilio langu,Ili nitangaze kazi zako zote.+

Maelezo ya Chini

Ao “wenye kujisifu.”
Ao “Tumbo lao limenenepa.”
Tnn., “Unono.”
Ao “eko.”
Tnn., “kizazi cha wana wako.”
Tnn., “utazarau.”
Tnn., “katika figo zangu.”
Tnn., “Utanyamazisha.”
Ao “kukosa uaminifu.”