Zaburi 47:1-9
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
47 Ninyi vikundi vyote vya watu, mupige mikono.
Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi pamoja na vigelegele vya shangwe.
2 Kwa maana Yehova Mwenye Kuwa Juu Zaidi ni mwenye kuogopesha sana;+
Yeye ndiye Mufalme mukubwa juu ya dunia yote.+
3 Anatiisha vikundi vya watu chini yetu;
Anatia mataifa chini ya miguu yetu.+
4 Anatuchagulia uriti wetu,+
Kiburi cha Yakobo, mwenye anapenda.+ (Sela)
5 Mungu amepanda juu katika vigelegele vya shangwe;
Yehova, katika sauti ya baragumu.*
6 Mumuimbie Mungu sifa,* muimbe sifa.
Mumuimbie sifa Mufalme wetu, muimbe sifa.
7 Kwa maana Mungu ni Mufalme wa dunia yote;+
Muimbe sifa, na muonyeshe ufahamu.
8 Mungu amekuwa Mufalme juu ya mataifa.+
Mungu anakaa kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.
9 Viongozi wa vikundi vya watu wamekusanyika pamoja
Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.
Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu.
Ameinuliwa sana.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “pembe ya kondoo-dume; tarumbeta.”
^ Ao “Mumupigie Mungu muziki.”
^ Tnn., “ngao za dunia ni za.”