Zaburi 47:1-9

  • Mungu ni Mufalme juu ya dunia yote

    • “Yehova ni mwenye kuogopesha sana” (2)

    • Mumuimbie Mungu sifa (6, 7)

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki. 47  Ninyi vikundi vyote vya watu, mupige mikono. Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi pamoja na vigelegele vya shangwe.   Kwa maana Yehova Mwenye Kuwa Juu Zaidi ni mwenye kuogopesha sana;+ Yeye ndiye Mufalme mukubwa juu ya dunia yote.+   Anatiisha vikundi vya watu chini yetu; Anatia mataifa chini ya miguu yetu.+   Anatuchagulia uriti wetu,+ Kiburi cha Yakobo, mwenye anapenda.+ (Sela)   Mungu amepanda juu katika vigelegele vya shangwe; Yehova, katika sauti ya baragumu.*   Mumuimbie Mungu sifa,* muimbe sifa. Mumuimbie sifa Mufalme wetu, muimbe sifa.   Kwa maana Mungu ni Mufalme wa dunia yote;+ Muimbe sifa, na muonyeshe ufahamu.   Mungu amekuwa Mufalme juu ya mataifa.+ Mungu anakaa kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.   Viongozi wa vikundi vya watu wamekusanyika pamoja Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu. Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu. Ameinuliwa sana.+

Maelezo ya Chini

Ao “pembe ya kondoo-dume; tarumbeta.”
Ao “Mumupigie Mungu muziki.”
Tnn., “ngao za dunia ni za.”