Zaburi 47:1-9
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki.
47 Ninyi vikundi vyote vya watu, mupige mikono.
Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi pamoja na vigelegele vya shangwe.
2 Kwa maana Yehova Mwenye Kuwa Juu Zaidi ni mwenye kuogopesha sana;+Yeye ndiye Mufalme mukubwa juu ya dunia yote.+
3 Anatiisha vikundi vya watu chini yetu;Anatia mataifa chini ya miguu yetu.+
4 Anatuchagulia uriti wetu,+Kiburi cha Yakobo, mwenye anapenda.+ (Sela)
5 Mungu amepanda juu katika vigelegele vya shangwe;Yehova, katika sauti ya baragumu.*
6 Mumuimbie Mungu sifa,* muimbe sifa.
Mumuimbie sifa Mufalme wetu, muimbe sifa.
7 Kwa maana Mungu ni Mufalme wa dunia yote;+Muimbe sifa, na muonyeshe ufahamu.
8 Mungu amekuwa Mufalme juu ya mataifa.+
Mungu anakaa kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.
9 Viongozi wa vikundi vya watu wamekusanyika pamojaPamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.
Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu.
Ameinuliwa sana.+

