Zaburi 47:1-9

  • Mungu ni Mufalme juu ya dunia yote

    • “Yehova ni mwenye kuogopesha sana” (2)

    • Mumuimbie Mungu sifa (6, 7)

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki. 47  Ninyi vikundi vyote vya watu, mupige mikono. Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi pamoja na vigelegele vya shangwe.  2  Kwa maana Yehova Mwenye Kuwa Juu Zaidi ni mwenye kuogopesha sana;+Yeye ndiye Mufalme mukubwa juu ya dunia yote.+  3  Anatiisha vikundi vya watu chini yetu;Anatia mataifa chini ya miguu yetu.+  4  Anatuchagulia uriti wetu,+Kiburi cha Yakobo, mwenye anapenda.+ (Sela)  5  Mungu amepanda juu katika vigelegele vya shangwe;Yehova, katika sauti ya baragumu.*  6  Mumuimbie Mungu sifa,* muimbe sifa. Mumuimbie sifa Mufalme wetu, muimbe sifa.  7  Kwa maana Mungu ni Mufalme wa dunia yote;+Muimbe sifa, na muonyeshe ufahamu.  8  Mungu amekuwa Mufalme juu ya mataifa.+ Mungu anakaa kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.  9  Viongozi wa vikundi vya watu wamekusanyika pamojaPamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu. Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu. Ameinuliwa sana.+

Maelezo ya Chini

Ao “pembe ya kondoo-dume; tarumbeta.”
Ao “Mumupigie Mungu muziki.”
Tnn., “ngao za dunia ni za.”