Zaburi 2:1-12
2 Sababu gani mataifa yako na musukosukoNa vikundi vya watu vinasema kwa sauti ya chini-chini* jambo lenye halina maana?+
2 Wafalme wa dunia wanajipangaNa maofisa wakubwa wanakusanyika* pamoja kama mutu mumoja+Ili kumupinga Yehova na ili kumupinga mutiwa-mafuta wake.*+
3 Wanasema: “Tukate pingu zaoNa kutupa kamba zao!”
4 Ule mwenye kukaa akiwa mufalme kule mbinguni atacheka;Yehova atawachekelea.
5 Wakati huo atasema nao katika kasirani yakeNa kuwaogopesha sana katika kasirani yake yenye kuwaka,
6 Kwa kusema: “Mimi mwenyewe nimemuweka mufalme wangu+Juu ya Sayuni,+ mulima wangu mutakatifu.”
7 Muache nitangaze agizo la Yehova;Aliniambia: “Wewe ni mwana wangu;+Leo nimekuwa baba yako.+
8 Uniombe, na nitakupatia mataifa kuwa uriti wakoNa miisho ya dunia kuwa mali yako.+
9 Utawavunja kwa fimbo ya ufalme ya chuma,+Na utawavunja-vunja kama chombo cha udongo.”+
10 Basi sasa, ninyi wafalme, muonyeshe ufahamu;Mukubali kurekebishwa,* ninyi waamuzi wa dunia.
11 Mumutumikie Yehova kwa woga,Na mushangilie mukitetemeka.
12 Mumuheshimie* mwana,+ kama hamufanye vile Mungu* atakasirika sanaNa ninyi mutaangamia kutoka katika njia,+Kwa maana kasirani Yake inawaka haraka.
Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.

