Zaburi 2:1-12

  • Yehova na mutiwa-mafuta wake

    • Yehova anacheka mataifa (4)

    • Yehova anamuweka mufalme wake (6)

    • Mumuheshimie mwana (12)

2  Sababu gani mataifa yako na musukosuko Na vikundi vya watu vinasema kwa sauti ya chini-chini* jambo lenye halina maana?+   Wafalme wa dunia wanajipanga Na maofisa wakubwa wanakusanyika* pamoja kama mutu mumoja+ Ili kumupinga Yehova na ili kumupinga mutiwa-mafuta wake.*+   Wanasema: “Tukate pingu zao Na kutupa kamba zao!”   Ule mwenye kukaa akiwa mufalme kule mbinguni atacheka; Yehova atawachekelea.   Wakati huo atasema nao katika kasirani yake Na kuwaogopesha sana katika kasirani yake yenye kuwaka,   Kwa kusema: “Mimi mwenyewe nimemuweka mufalme wangu+ Juu ya Sayuni,+ mulima wangu mutakatifu.”   Muache nitangaze agizo la Yehova; Aliniambia: “Wewe ni mwana wangu;+ Leo nimekuwa baba yako.+   Uniombe, na nitakupatia mataifa kuwa uriti wako Na miisho ya dunia kuwa mali yako.+   Utawavunja kwa fimbo ya ufalme ya chuma,+ Na utawavunja-vunja kama chombo cha udongo.”+ 10  Basi sasa, ninyi wafalme, muonyeshe ufahamu; Mukubali kurekebishwa,* ninyi waamuzi wa dunia. 11  Mumutumikie Yehova kwa woga, Na mushangilie mukitetemeka. 12  Mumuheshimie* mwana,+ kama hamufanye vile Mungu* atakasirika sana Na ninyi mutaangamia kutoka katika njia,+ Kwa maana kasirani Yake inawaka haraka. Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.

Maelezo ya Chini

Ao “vinatafakari juu ya; vinafikiri sana juu ya.”
Ao “wanafanya shauri pamoja.”
Ao “Kristo wake.”
Ao “Muonywe.”
Tnn., “Mumubusu.”
Tnn., “yeye.”