Zaburi 2:1-12

  • Yehova na mutiwa-mafuta wake

    • Yehova anacheka mataifa (4)

    • Yehova anamuweka mufalme wake (6)

    • Mumuheshimie mwana (12)

2  Sababu gani mataifa yako na musukosukoNa vikundi vya watu vinasema kwa sauti ya chini-chini* jambo lenye halina maana?+  2  Wafalme wa dunia wanajipangaNa maofisa wakubwa wanakusanyika* pamoja kama mutu mumoja+Ili kumupinga Yehova na ili kumupinga mutiwa-mafuta wake.*+  3  Wanasema: “Tukate pingu zaoNa kutupa kamba zao!”  4  Ule mwenye kukaa akiwa mufalme kule mbinguni atacheka;Yehova atawachekelea.  5  Wakati huo atasema nao katika kasirani yakeNa kuwaogopesha sana katika kasirani yake yenye kuwaka,  6  Kwa kusema: “Mimi mwenyewe nimemuweka mufalme wangu+Juu ya Sayuni,+ mulima wangu mutakatifu.”  7  Muache nitangaze agizo la Yehova;Aliniambia: “Wewe ni mwana wangu;+Leo nimekuwa baba yako.+  8  Uniombe, na nitakupatia mataifa kuwa uriti wakoNa miisho ya dunia kuwa mali yako.+  9  Utawavunja kwa fimbo ya ufalme ya chuma,+Na utawavunja-vunja kama chombo cha udongo.”+ 10  Basi sasa, ninyi wafalme, muonyeshe ufahamu;Mukubali kurekebishwa,* ninyi waamuzi wa dunia. 11  Mumutumikie Yehova kwa woga,Na mushangilie mukitetemeka. 12  Mumuheshimie* mwana,+ kama hamufanye vile Mungu* atakasirika sanaNa ninyi mutaangamia kutoka katika njia,+Kwa maana kasirani Yake inawaka haraka. Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.

Maelezo ya Chini

Ao “vinatafakari juu ya; vinafikiri sana juu ya.”
Ao “wanafanya shauri pamoja.”
Ao “Kristo wake.”
Ao “Muonywe.”
Tnn., “Mumubusu.”
Tnn., “yeye.”