Zaburi 39:1-13
Kwa kiongozi; wa Yedutuni.*+ Muziki wa Daudi.
39 Nilisema: “Nitalinda hatua yangu
Ili niepuke kutenda zambi kwa ulimi wangu.+
Nitalinda kinywa changu kwa kitu cha kufunga kinywa+
Wakati wote wenye mutu yeyote muovu iko* mbele yangu.”
2 Nilikuwa bubu na nilikuwa kimya;+
Niliendelea kunyamaza hata kuhusu mambo ya muzuri,
Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*
3 Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu.
Wakati nilikuwa ninafikiri sana,* moto huo uliendelea kuwaka.
Kisha ulimi wangu ukasema:
4 “Ee Yehova, unisaidie kujua namna mwisho wangu utakuwa,
Na kipimo cha siku zangu,+
Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*
5 Kwa kweli, umefanya siku zangu zikuwe kidogo tu;*+
Na urefu wa maisha yangu hauko kitu mbele yako.+
Hakika kila mwanadamu, hata kama anaonekana kuwa salama, haiko kitu lakini pumuzi tu.+ (Sela)
6 Hakika kila mwanadamu anatembea huku na huku kama kivuli.
Anakimbia huku na huku* bila sababu.
Anarundika mali, bila kujua ni nani ataifurahia.+
7 Basi, ninaweza kutumainia nini, Ee Yehova?
Wewe ndiye tumaini langu pekee.
8 Uniokoe katika makosa yangu yote.+
Usiruhusu mupumbavu anifanye kuwa kitu cha kuzarauliwa.
9 Niliendelea kuwa bubu;
Sikuweza kufungua kinywa changu,+
Kwa maana wewe ndiye ulifanya vile.+
10 Uniondolee pigo lako.
Nimekuwa muzaifu kabisa kwa sababu mukono wako unanipiga.
11 Unamurekebisha mwanadamu kwa kumupatia azabu kwa sababu ya kosa lake;+
Unaharibu kabisa vitu vyenye anapenda sana kama vile nondo* anaharibu.
Hakika kila mwanadamu ni pumuzi tu.+ (Sela)
12 Sikia sala yangu, Ee Yehova,
Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada.+
Usijifanye kuwa hauone machozi yangu.
Kwa maana mimi niko mukaaji mugeni tu mbele yako,+
Musafiri mwenye kupita,* kama vile mababu zangu wote.+
13 Ondoa macho yako ya ukali juu yangu ili nichangamuke
Mbele nikufe na kupotea.”
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “eko.”
^ Ao “yalichochewa.”
^ Tnn., “uliwaka moto.”
^ Ao “ninalia kwa maumivu.”
^ Ao “nijue namna ninapita haraka.”
^ Tnn., “zikuwe viganja vya mukono.”
^ Tnn., “Anafanya fujo.”
^ Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
^ Ao “Muhamiaji.”