Zaburi 39:1-13

  • Ufupi wa maisha

    • Mwanadamu ni pumuzi tu (5, 11)

    • “Usijifanye kuwa hauone machozi yangu” (12)

Kwa kiongozi; wa Yedutuni.*+ Muziki wa Daudi. 39  Nilisema: “Nitalinda hatua yangu Ili niepuke kutenda zambi kwa ulimi wangu.+ Nitalinda kinywa changu kwa kitu cha kufunga kinywa+ Wakati wote wenye mutu yeyote muovu iko* mbele yangu.”   Nilikuwa bubu na nilikuwa kimya;+ Niliendelea kunyamaza hata kuhusu mambo ya muzuri, Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*   Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu. Wakati nilikuwa ninafikiri sana,* moto huo uliendelea kuwaka. Kisha ulimi wangu ukasema:   “Ee Yehova, unisaidie kujua namna mwisho wangu utakuwa, Na kipimo cha siku zangu,+ Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*   Kwa kweli, umefanya siku zangu zikuwe kidogo tu;*+ Na urefu wa maisha yangu hauko kitu mbele yako.+ Hakika kila mwanadamu, hata kama anaonekana kuwa salama, haiko kitu lakini pumuzi tu.+ (Sela)   Hakika kila mwanadamu anatembea huku na huku kama kivuli. Anakimbia huku na huku* bila sababu. Anarundika mali, bila kujua ni nani ataifurahia.+   Basi, ninaweza kutumainia nini, Ee Yehova? Wewe ndiye tumaini langu pekee.   Uniokoe katika makosa yangu yote.+ Usiruhusu mupumbavu anifanye kuwa kitu cha kuzarauliwa.   Niliendelea kuwa bubu; Sikuweza kufungua kinywa changu,+ Kwa maana wewe ndiye ulifanya vile.+ 10  Uniondolee pigo lako. Nimekuwa muzaifu kabisa kwa sababu mukono wako unanipiga. 11  Unamurekebisha mwanadamu kwa kumupatia azabu kwa sababu ya kosa lake;+ Unaharibu kabisa vitu vyenye anapenda sana kama vile nondo* anaharibu. Hakika kila mwanadamu ni pumuzi tu.+ (Sela) 12  Sikia sala yangu, Ee Yehova, Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada.+ Usijifanye kuwa hauone machozi yangu. Kwa maana mimi niko mukaaji mugeni tu mbele yako,+ Musafiri mwenye kupita,* kama vile mababu zangu wote.+ 13  Ondoa macho yako ya ukali juu yangu ili nichangamuke Mbele nikufe na kupotea.”

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “yalichochewa.”
Tnn., “uliwaka moto.”
Ao “ninalia kwa maumivu.”
Ao “nijue namna ninapita haraka.”
Tnn., “zikuwe viganja vya mukono.”
Tnn., “Anafanya fujo.”
Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
Ao “Muhamiaji.”