Zaburi 51:1-19

  • Sala ya mutu mwenye alitubu

    • Mwenye zambi tangu wakati mama yake alichukua mimba yake (5)

    • “Unisafishe kutokana na zambi yangu” (7)

    • “Umba moyo safi ndani yangu” (10)

    • Moyo wenye kupondwa unamupendeza Mungu (17)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, wakati nabii Natani alikuja kwa Daudi kisha yeye kulala na Bat-sheba.+ 51  Unionyeshe wema, Ee Mungu, kulingana na upendo wako mushikamanifu.+ Futa makosa yangu kulingana na rehema yako kubwa.+   Unioshe kabisa kutokana na kosa langu,+ Na unisafishe kutokana na zambi yangu.+   Kwa maana ninajua muzuri makosa yangu, Na zambi yangu iko mbele yangu* sikuzote.+   Kukuelekea wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda zambi;+ Nimetenda mambo ya mubaya mbele ya macho yako.+ Kwa hiyo, uko mwenye haki wakati unasema, Uko mwenye haki katika hukumu yako.+   Angalia! Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa, Na mama yangu alichukua mimba yangu katika zambi.*+   Angalia! Unapendezwa na kweli katika mutu wa ndani;+ Fundisha mutu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.   Unisafishe kutokana na zambi yangu kwa hisopo, ili nikuwe safi;+ Unioshe, ili nikuwe mweupe kuliko teluji.*+   Acha nisikie sauti za shangwe na furaha, Ili mifupa yenye uliponda ishangilie.+   Geuzia uso wako mbali* na zambi zangu,+ Na ufutilie mbali* makosa yangu yote.+ 10  Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+ Na utie ndani yangu roho mupya,+ yenye kuwa imara. 11  Usinitupe kutoka mbele yako; Wala usiondoe roho yako takatifu juu yangu. 12  Unirudishie shangwe ya wokovu wako;+ Uchochee ndani yangu utayari wa kukutii.* 13  Nitafundisha wakosaji njia zako,+ Ili watenda-zambi warudie kwako. 14  Uniokoe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+ Ili ulimi wangu utangaze kwa shangwe haki yako.+ 15  Ee Yehova, fungua midomo yangu, Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+ 16  Kwa maana hautaki zabihu—kama ungeitaka ningeitoa;+ Haufurahie toleo nzima la kuteketezwa.+ 17  Zabihu zenye zinamupendeza Mungu ni roho yenye kuvunjika; Moyo wenye kuvunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautaukataa.*+ 18  Kwa nia yako njema tendea Sayuni mambo mema; Jenga kuta za Yerusalemu. 19  Halafu utafurahia zabihu za haki, Zabihu za kuteketezwa na matoleo mazima; Kisha ngombe-dume watatolewa kwenye mazabahu yako.+

Maelezo ya Chini

Ao “katika akili yangu.”
Tnn., “wewe tu.”
Ao “Na nilikuwa na zambi tangu wakati mama yangu alichukua mimba yangu.”
Ao “mutu wangu mwenye kuwa katika siri.”
Ao “neige.”
Ao “Ficha uso wako mbali.”
Ao “ufute.”
Tnn., “Unitegemeze kwa kunipatia roho yenye kuwa tayari.”
Ao “hautauzarau.”