Zaburi 51:1-19
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, wakati nabii Natani alikuja kwa Daudi kisha yeye kulala na Bat-sheba.+
51 Unionyeshe wema, Ee Mungu, kulingana na upendo wako mushikamanifu.+
Futa makosa yangu kulingana na rehema yako kubwa.+
2 Unioshe kabisa kutokana na kosa langu,+Na unisafishe kutokana na zambi yangu.+
3 Kwa maana ninajua muzuri makosa yangu,Na zambi yangu iko mbele yangu* sikuzote.+
4 Kukuelekea wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda zambi;+Nimetenda mambo ya mubaya mbele ya macho yako.+
Kwa hiyo, uko mwenye haki wakati unasema,Uko mwenye haki katika hukumu yako.+
5 Angalia! Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa,Na mama yangu alichukua mimba yangu katika zambi.*+
6 Angalia! Unapendezwa na kweli katika mutu wa ndani;+Fundisha mutu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.
7 Unisafishe kutokana na zambi yangu kwa hisopo, ili nikuwe safi;+Unioshe, ili nikuwe mweupe kuliko teluji.*+
8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,Ili mifupa yenye uliponda ishangilie.+
9 Geuzia uso wako mbali* na zambi zangu,+Na ufutilie mbali* makosa yangu yote.+
10 Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+Na utie ndani yangu roho mupya,+ yenye kuwa imara.
11 Usinitupe kutoka mbele yako;Wala usiondoe roho yako takatifu juu yangu.
12 Unirudishie shangwe ya wokovu wako;+Uchochee ndani yangu utayari wa kukutii.*
13 Nitafundisha wakosaji njia zako,+Ili watenda-zambi warudie kwako.
14 Uniokoe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+Ili ulimi wangu utangaze kwa shangwe haki yako.+
15 Ee Yehova, fungua midomo yangu,Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+
16 Kwa maana hautaki zabihu—kama ungeitaka ningeitoa;+Haufurahie toleo nzima la kuteketezwa.+
17 Zabihu zenye zinamupendeza Mungu ni roho yenye kuvunjika;Moyo wenye kuvunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautaukataa.*+
18 Kwa nia yako njema tendea Sayuni mambo mema;Jenga kuta za Yerusalemu.
19 Halafu utafurahia zabihu za haki,Zabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;Kisha ngombe-dume watatolewa kwenye mazabahu yako.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “katika akili yangu.”
^ Tnn., “wewe tu.”
^ Ao “Na nilikuwa na zambi tangu wakati mama yangu alichukua mimba yangu.”
^ Ao “mutu wangu mwenye kuwa katika siri.”
^ Ao “neige.”
^ Ao “Ficha uso wako mbali.”
^ Ao “ufute.”
^ Tnn., “Unitegemeze kwa kunipatia roho yenye kuwa tayari.”
^ Ao “hautauzarau.”

