Zaburi 21:1-13

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 21  Ee Yehova, mfalme hushangilia katika nguvu zako;+Na katika wokovu wako jinsi anavyotaka kuwa na shangwe sana!+   Tamaa ya moyo wake umempa,+Na matakwa ya midomo yake hukuyazuilia.+ Sela.   Kwa maana ulikutana naye ukiwa na baraka za mema,+Na kumvika taji la dhahabu safi kichwani.+   Alikuomba uhai. Ukampa huo,+Urefu wa siku mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+   Utukufu wake ni mkuu katika wokovu wako.+Heshima na fahari unaweka juu yake.+   Kwa maana umemfanya abarikiwe sana milele;+Unamfanya afurahie kwa shangwe mbele za uso wako.+   Kwa maana mfalme anategemea Yehova,+Naam, fadhili zenye upendo za Aliye Juu Zaidi. Hatatikiswa.+   Mkono wako utawapata adui zako wote;+Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.   Utawafanya wawe kama tanuru yenye moto wakati wako uliowekwa wa kukaza uangalifu wako;+Yehova atawameza katika hasira yake, na moto utawateketeza.+ 10  Utaangamiza wazaliwa wao kutoka duniani,+Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu.+ 11  Kwa maana wamekuelekezea mabaya;+Wametunga mawazo wasiyoweza kutimiza.+ 12  Kwa maana utawafanya wageuze migongo yao kwa kukimbia+Kwa nyuzi za upinde wako ambazo unatayarisha dhidi ya nyuso zao.+ 13  Na utukuzwe katika nguvu zako, Ee Yehova.+Tutaimba na kuzipigia muziki nguvu zako.+

Maelezo ya Chini