Zaburi 21:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
21 Ee Yehova, mfalme hushangilia katika nguvu zako;+Na katika wokovu wako jinsi anavyotaka kuwa na shangwe sana!+
2 Tamaa ya moyo wake umempa,+Na matakwa ya midomo yake hukuyazuilia.+ Sela.
3 Kwa maana ulikutana naye ukiwa na baraka za mema,+Na kumvika taji la dhahabu safi kichwani.+
4 Alikuomba uhai. Ukampa huo,+Urefu wa siku mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
5 Utukufu wake ni mkuu katika wokovu wako.+Heshima na fahari unaweka juu yake.+
6 Kwa maana umemfanya abarikiwe sana milele;+Unamfanya afurahie kwa shangwe mbele za uso wako.+
7 Kwa maana mfalme anategemea Yehova,+Naam, fadhili zenye upendo za Aliye Juu Zaidi. Hatatikiswa.+
8 Mkono wako utawapata adui zako wote;+Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.
9 Utawafanya wawe kama tanuru yenye moto wakati wako uliowekwa wa kukaza uangalifu wako;+Yehova atawameza katika hasira yake, na moto utawateketeza.+
10 Utaangamiza wazaliwa wao kutoka duniani,+Na uzao wao kutoka kati ya wana wa binadamu.+
11 Kwa maana wamekuelekezea mabaya;+Wametunga mawazo wasiyoweza kutimiza.+
12 Kwa maana utawafanya wageuze migongo yao kwa kukimbia+Kwa nyuzi za upinde wako ambazo unatayarisha dhidi ya nyuso zao.+
13 Na utukuzwe katika nguvu zako, Ee Yehova.+Tutaimba na kuzipigia muziki nguvu zako.+