Zaburi 18:1-50

Kwa kiongozi. Wa mtumishi wa Yehova, wa Daudi, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka mkononi mwa adui zake wote na kutoka mkononi mwa Sauli.+ Naye akasema: 18  Nitakupenda wewe, Ee Yehova nguvu zangu.+   Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu.+Mungu wangu ni mwamba wangu. Nitamkimbilia,+Ngao yangu na pembe yangu ya wokovu, kilele changu salama.+   Nitamwita, Yehova, Yule anayestahili kusifiwa,+Nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.+   Kamba za kifo zilinizunguka;+Mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu pia yaliendelea kuniogopesha.+   Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+Mitego ya kifo ilinikabili.+   Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+   Na dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka,+Nayo misingi ya milima ikasukasuka,+Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+   Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, nao moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+Makaa yakawaka moto kutoka kwake.   Naye akaziinamisha mbingu, akashuka.+Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake. 10  Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi, akaja akiwa anaruka,+Naye akaja akiruka juu ya mabawa ya roho.+ 11  Kisha akalifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha,+Kama kibanda cha kumzunguka pande zote, Maji yenye giza, mawingu mazito.+ 12  Kutoka katika mwangaza ulio mbele yake kulikuwa na mawingu yake yaliyopita,+Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.+ 13  Na mbinguni Yehova akaanza kunguruma,+Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake,+Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto. 14  Naye akaendelea kuitupa mishale yake, ili awatawanye;+Naye akatupa umeme, ili awavuruge.+ 15  Na sakafu za vijito vya maji zikaonekana,+Na misingi ya nchi yenye kuzaa ikafunuliwa,+Kwa kemeo lako, Ee Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yako.+ 16  Alikuwa akituma mkono kutoka juu, alikuwa akinichukua,+Alikuwa akinitoa ndani ya maji makuu.+ 17  Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Na kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+ 18  Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+Lakini Yehova akawa kama tegemeo kwa ajili yangu.+ 19  Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+ 20  Yehova hunipa thawabu kulingana na uadilifu wangu;+Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+ 21  Kwa maana nimezishika njia za Yehova,+Wala kwa uovu sikuondoka kwa Mungu wangu.+ 22  Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu yako mbele yangu,+Nazo sheria zake sitaziondoa kutoka kwangu.+ 23  Nami nitajiendesha bila kosa mbele zake,+Nami nitajiepusha na kosa.+ 24  Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele za macho yake.+ 25  Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mwanamume asiye na kosa, wewe utatenda kwa njia isiyo na kosa;+ 26  Kwa mtu anayebaki safi utakuwa safi;+Na kwa mpotovu utakuwa mwenye hila;+ 27  Kwa sababu watu wenye kuteseka wewe mwenyewe utawaokoa;+Bali macho yenye majivuno utayashusha.+ 28  Kwa maana wewe mwenyewe utaiwasha taa yangu, Ee Yehova;+Mungu wangu atafanya giza langu liangaze.+ 29  Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+Na kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+ 30  Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+Neno la Yehova limetakaswa.+Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+ 31  Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+Na ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?+ 32  Mungu wa kweli Ndiye anayenifunga sana mshipi wa nguvu,+Naye ataifanya njia yangu kuwa kamilifu,+ 33  Kuifanya miguu yangu iwe kama ya paa,+Na kwenye mahali palipo juu kwangu yeye huendelea kunisimamisha.+ 34  Anaifundisha mikono yangu kupigana vita,+Na mikono yangu imepinda upinde wa shaba.+ 35  Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+Na mkono wako mwenyewe wa kuume utanitegemeza,+Na unyenyekevu wako mwenyewe utanifanya kuwa mkuu.+ 36  Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu,+Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+ 37  Nitawafuatilia adui zangu na kuwafikia;Nami sitarudi mpaka waangamizwe.+ 38  Nitawavunja vipande-vipande hivi kwamba wasiweze kusimama;+Wataanguka chini ya miguu yangu.+ 39  Nawe utanifunga mshipi wa nguvu kwa ajili ya vita;Utawaangusha chini yangu wale wanaoniinukia.+ 40  Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo zao;+Nao wale wanaonichukia vikali, nitawanyamazisha.+ 41  Wanalia wapate msaada, lakini hakuna mwokozi,+Kwa Yehova, lakini yeye hawajibu.+ 42  Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi mbele ya upepo;+Nitawamwaga kama matope ya barabarani.+ 43  Utaniokoa kutokana na watu wenye kutafuta-tafuta makosa.+Utanichagua kuwa kiongozi wa mataifa.+ Watu ambao sijawajua​​—⁠watanitumikia.+ 44  Kwa kusikia fununu tu watanitii;+Wageni watanijia wakitetemeka.+ 45  Wageni watakuwa dhaifu,Nao watakuja wakitetemeka kutoka katika maboma yao.+ 46  Yehova anaishi,+ na abarikiwe Mwamba wangu,+Na Mungu wa wokovu wangu atukuzwe.+ 47  Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu;+Naye hutiisha vikundi vya watu chini yangu.+ 48  Ananiokoa kutoka kwa adui zangu wenye hasira;+Utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu,+Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye jeuri.+ 49  Ndiyo sababu nitakusifu wewe kati ya mataifa, Ee Yehova,+Nami nitalipigia jina lako muziki.+ 50  Yeye anafanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.