Zaburi 18:1-50
Kwa kiongozi. Wa mtumishi wa Yehova, wa Daudi, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka mkononi mwa adui zake wote na kutoka mkononi mwa Sauli.+ Naye akasema:
18 Nitakupenda wewe, Ee Yehova nguvu zangu.+
2 Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu.+Mungu wangu ni mwamba wangu. Nitamkimbilia,+Ngao yangu na pembe yangu ya wokovu, kilele changu salama.+
3 Nitamwita, Yehova, Yule anayestahili kusifiwa,+Nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.+
4 Kamba za kifo zilinizunguka;+Mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu pia yaliendelea kuniogopesha.+
5 Kamba za Kaburi* zilinizunguka;+Mitego ya kifo ilinikabili.+
6 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+
7 Na dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka,+Nayo misingi ya milima ikasukasuka,+Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, nao moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+Makaa yakawaka moto kutoka kwake.
9 Naye akaziinamisha mbingu, akashuka.+Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi, akaja akiwa anaruka,+Naye akaja akiruka juu ya mabawa ya roho.+
11 Kisha akalifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha,+Kama kibanda cha kumzunguka pande zote,
Maji yenye giza, mawingu mazito.+
12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele yake kulikuwa na mawingu yake yaliyopita,+Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.+
13 Na mbinguni Yehova akaanza kunguruma,+Na Aliye Juu Zaidi akaanza kutoa sauti yake,+Mvua ya mawe na makaa yanayowaka moto.
14 Naye akaendelea kuitupa mishale yake, ili awatawanye;+Naye akatupa umeme, ili awavuruge.+
15 Na sakafu za vijito vya maji zikaonekana,+Na misingi ya nchi yenye kuzaa ikafunuliwa,+Kwa kemeo lako, Ee Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yako.+
16 Alikuwa akituma mkono kutoka juu, alikuwa akinichukua,+Alikuwa akinitoa ndani ya maji makuu.+
17 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+Na kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
18 Waliendelea kunikabili katika siku ya msiba wangu,+Lakini Yehova akawa kama tegemeo kwa ajili yangu.+
19 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
20 Yehova hunipa thawabu kulingana na uadilifu wangu;+Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+
21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,+Wala kwa uovu sikuondoka kwa Mungu wangu.+
22 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu yako mbele yangu,+Nazo sheria zake sitaziondoa kutoka kwangu.+
23 Nami nitajiendesha bila kosa mbele zake,+Nami nitajiepusha na kosa.+
24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele za macho yake.+
25 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+Kwa mwanamume asiye na kosa, wewe utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
26 Kwa mtu anayebaki safi utakuwa safi;+Na kwa mpotovu utakuwa mwenye hila;+
27 Kwa sababu watu wenye kuteseka wewe mwenyewe utawaokoa;+Bali macho yenye majivuno utayashusha.+
28 Kwa maana wewe mwenyewe utaiwasha taa yangu, Ee Yehova;+Mungu wangu atafanya giza langu liangaze.+
29 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+Na kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
30 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+Neno la Yehova limetakaswa.+Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+Na ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?+
32 Mungu wa kweli Ndiye anayenifunga sana mshipi wa nguvu,+Naye ataifanya njia yangu kuwa kamilifu,+
33 Kuifanya miguu yangu iwe kama ya paa,+Na kwenye mahali palipo juu kwangu yeye huendelea kunisimamisha.+
34 Anaifundisha mikono yangu kupigana vita,+Na mikono yangu imepinda upinde wa shaba.+
35 Nawe utanipa ngao yako ya wokovu,+Na mkono wako mwenyewe wa kuume utanitegemeza,+Na unyenyekevu wako mwenyewe utanifanya kuwa mkuu.+
36 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu,+Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
37 Nitawafuatilia adui zangu na kuwafikia;Nami sitarudi mpaka waangamizwe.+
38 Nitawavunja vipande-vipande hivi kwamba wasiweze kusimama;+Wataanguka chini ya miguu yangu.+
39 Nawe utanifunga mshipi wa nguvu kwa ajili ya vita;Utawaangusha chini yangu wale wanaoniinukia.+
40 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo zao;+Nao wale wanaonichukia vikali, nitawanyamazisha.+
41 Wanalia wapate msaada, lakini hakuna mwokozi,+Kwa Yehova, lakini yeye hawajibu.+
42 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi mbele ya upepo;+Nitawamwaga kama matope ya barabarani.+
43 Utaniokoa kutokana na watu wenye kutafuta-tafuta makosa.+Utanichagua kuwa kiongozi wa mataifa.+
Watu ambao sijawajua—watanitumikia.+
44 Kwa kusikia fununu tu watanitii;+Wageni watanijia wakitetemeka.+
45 Wageni watakuwa dhaifu,Nao watakuja wakitetemeka kutoka katika maboma yao.+
46 Yehova anaishi,+ na abarikiwe Mwamba wangu,+Na Mungu wa wokovu wangu atukuzwe.+
47 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu;+Naye hutiisha vikundi vya watu chini yangu.+
48 Ananiokoa kutoka kwa adui zangu wenye hasira;+Utaniinua juu ya wale wanaosimama dhidi yangu,+Utanikomboa kutoka kwa mtu mwenye jeuri.+
49 Ndiyo sababu nitakusifu wewe kati ya mataifa, Ee Yehova,+Nami nitalipigia jina lako muziki.+
50 Yeye anafanya matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake+Na kuonyesha fadhili zenye upendo kwa mtiwa-mafuta wake,+Kwa Daudi na kwa uzao wake mpaka wakati usio na kipimo.+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.