Zaburi 52:1-9
Kwa kiongozi. Maskili. Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Kwa nini unajisifia yaliyo mabaya, ewe mwenye nguvu?+Fadhili zenye upendo za Mungu ni za mchana kutwa.+
2 Ulimi wako hupanga hila za kuleta shida, ukiwa umenolewa kama wembe,+Ukifanya kazi kwa udanganyifu.+
3 Umependa yaliyo mabaya kuliko yaliyo mema,+Kusema uwongo kuliko kusema yaliyo ya uadilifu.+ Sela.
4 Umependa maneno yote yenye kumeza,+Ewe ulimi wenye udanganyifu.+
5 Mungu mwenyewe pia atakubomoa milele;+Atakupiga na kukuangusha na kukurarua kutoka katika hema lako,+Naye atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ Sela.
6 Nao waadilifu wataona hilo na kuogopa,+Nao watamcheka.+
7 Huyo ndiye mwanamume ambaye hamweki Mungu kuwa ngome yake,+Lakini anategemea wingi wa utajiri wake,+Ambaye hulindwa kutokana na shida anazoleta.+
8 Lakini nitakuwa kama mzeituni+ wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;Nazitegemea fadhili zenye upendo za Mungu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
9 Nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, kwa maana wewe umechukua hatua;+Nami nitalitumainia jina lako, kwa sababu ni jema, mbele ya washikamanifu wako.+