Zaburi 58:1-11
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.
58 Katika kimya chenu je, kweli mnaweza kusema juu ya uadilifu?+Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wana wa binadamu?+
2 Badala yake, kwa moyo mnafanya mambo ambayo ni ya kukosa uadilifu kabisa duniani,+Na kutayarisha barabara kwa ajili ya jeuri ya mikono yenu!+
3 Waovu wamekuwa wapotovu kutoka katika tumbo la uzazi;+Wametanga-tanga tangu tumboni na kuendelea;Wanasema uwongo.+
4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka,+Viziwi kama swila anayeziba sikio lake,+
5 Ambaye hataisikiliza sauti ya watumbuizaji,+Ingawa mtu mwenye hekima anapiga mafundo kwa uganga.+
6 Ee Mungu, yang’oe meno yaliyo kinywani mwao.+Uvunje mifupa ya taya za wana-simba wenye manyoya shingoni, Ee Yehova.
7 Na wayeyuke kana kwamba ni ndani ya maji yanayoenda zake;+Na aupinde upinde kwa ajili ya mishale yake huku wanapoanguka.+
8 Anatembea kama konokono anayeyeyuka;Kama mimba ya mwanamke iliyoharibika hakika hawataliona jua.+
9 Kabla vyungu vyenu havijapatwa na mkwamba uliowashwa,+Ulio mbichi na pia ule unaowaka, ataipeperusha kama upepo wa dhoruba.+
10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ameona kisasi.+Ataosha miguu yake katika damu ya mwovu.+
11 Nao wanadamu watasema:+ “Kwa kweli kuna matunda kwa ajili ya mwadilifu.+Kwa kweli kuna Mungu ambaye anahukumu duniani.”+