Zaburi 26:1-12
Ya Daudi.
26 Unihukumu,+ Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu,+Nami nimemtumaini Yehova, nisipate kutikisika.+
2 Unichunguze, Ee Yehova, na kunijaribu;+Usafishe figo zangu na moyo wangu.+
3 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ziko mbele ya macho yangu,Nami nimetembea katika kweli yako.+
4 Sikuketi na watu wasiosema kweli;+Wala siingii pamoja na wale wanaoficha jinsi walivyo.+
5 Nimelichukia kutaniko la watenda-maovu,+Wala siketi pamoja na waovu.+
6 Nitaiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia,+Nami nitatembea nikizunguka madhabahu yako, Ee Yehova,+
7 Ili kufanya utoaji shukrani usikiwe kwa sauti kubwa,+Na kutangaza kazi zako zote za ajabu.+
8 Yehova, nimependa makao ya nyumba yako+Na mahali ambapo utukufu wako hukaa.+
9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda-dhambi,+Wala uhai wangu pamoja na watu wenye hatia ya damu,+
10 Ambao mikononi mwao wana mwenendo mpotovu,+Na ambao mkono wao wa kuume umejaa rushwa.+
11 Mimi nami nitatembea katika utimilifu wangu.+Ee unikomboe+ na kunionyesha kibali.+
12 Mguu wangu utasimama mahali tambarare;+Kati ya makundi yaliyokutanika nitambariki Yehova.+