Zaburi 26:1-12

Ya Daudi. 26  Unihukumu,+ Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu,+Nami nimemtumaini Yehova, nisipate kutikisika.+   Unichunguze, Ee Yehova, na kunijaribu;+Usafishe figo zangu na moyo wangu.+   Kwa maana fadhili zako zenye upendo ziko mbele ya macho yangu,Nami nimetembea katika kweli yako.+   Sikuketi na watu wasiosema kweli;+Wala siingii pamoja na wale wanaoficha jinsi walivyo.+   Nimelichukia kutaniko la watenda-maovu,+Wala siketi pamoja na waovu.+   Nitaiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia,+Nami nitatembea nikizunguka madhabahu yako, Ee Yehova,+   Ili kufanya utoaji shukrani usikiwe kwa sauti kubwa,+Na kutangaza kazi zako zote za ajabu.+   Yehova, nimependa makao ya nyumba yako+Na mahali ambapo utukufu wako hukaa.+   Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda-dhambi,+Wala uhai wangu pamoja na watu wenye hatia ya damu,+ 10  Ambao mikononi mwao wana mwenendo mpotovu,+Na ambao mkono wao wa kuume umejaa rushwa.+ 11  Mimi nami nitatembea katika utimilifu wangu.+Ee unikomboe+ na kunionyesha kibali.+ 12  Mguu wangu utasimama mahali tambarare;+Kati ya makundi yaliyokutanika nitambariki Yehova.+

Maelezo ya Chini