Hamia kwenye habari

Mistari ya Biblia Yafafanuliwa

Tambua maana halisi ya mistari na misemo fulani ya Biblia inayojulikana sana. Jifunze mambo yaliyohusika katika mistari hiyo kwa kusoma muktadha wake. Ongeza uelewaji wako kwa msaada wa maelezo ya chini yanayofafanua maana na marejezo kwenye Biblia.

Mwanzo 1:1 Yafafanuliwa​—“Hapo Mwanzo Mungu Aliumba Mbingu na Dunia”

Ni kweli gani mbili muhimu ambazo zinatajwa katika mstari huu wa kwanza katika Biblia?

Kutoka 20:12 Yafafanuliwa​—“Mheshimu Baba Yako na Mama Yako”

Kwa kuongeza ahadi kwenye amri hiyio, Mungu alitoa kichocheo cha ziada cha kutii.

Yoshua 1:9 Yafafanuliwa​—“Uwe Jasiri na Imara”

Unawezaje kuwa jasiri na imara unapokabili changamoto na kulemewa na matatizo mengi?

Zaburi 23:4 Yafafanuliwa​—“Nijapopita Kati ya Bonde la Uvuli wa Mauti”

Mungu huwalindaje waabudu wake hata wanapokabili hali ngumu zaidi maishani mwao?

Zaburi 37:4 Yafafanuliwa​—“Uitafute Furaha Yako kwa Mwenyezi-Mungu”

Zaburi hii inatusaidiaje kujipatia hekima na kuwa aina ya watu ambao Mungu anakubali?

Zaburi 46:10 Yafafanuliwa​—“Acheni, Mjue ya Kuwa Mimi Ni Mungu”

Je, mstari huu unamaanisha tu kunyamaza kanisani?

Methali 3:5, 6 Yafafanuliwa​—“Usizitegemee Akili Zako Mwenyewe”

Unaweza kuonyeshaje kwamba unamtegemea Mungu badala ya kujitegemea mwenyewe?

Mithali 16:3 Yafafanuliwa​—“Mkabidhi BWANA Kazi Zako”

Kuna sababu gani mbili kwa nini wanadamu wanapaswa kutafuta mwongozo wa Mungu wanapofanya maamuzi?

Methali 22:6 Yafafanuliwa​—“Mlee Mtoto Katika Njia Impasayo”

Mtoto anapaswa kwenda katika “njia” gani? Je, kila mtu ana njia yake?

Mhubiri 3:11 Yafafanuliwa​—“Amefanya Kila Kitu Kipendeze kwa Wakati Wake”

Kazi za Mungu zinazopendeza zinatia ndani uumbaji wake na pia mambo mengine. Hilo linakuhusuje?

Isaya 26:3 Yafafanuliwa​—“Utamlinda Yeye Ambaye Moyo Wake Umekutegemea Katika Amani Kamilifu”

Je, kweli inawezekana kuwa na amani kamilifu? Inamaanisha nini kumtegemea Mungu kikamili?

Isaya 40:31 Yafafanuliwa—“Wale Wanaomtumaini Yehova Watapata Nguvu Tena”

Kwa nini Maandiko yanalinganisha tai anayepaa na mtu anayepata nguvu kutoka kwa Mungu?

Isaya 41:10 Yafafanuliwa—“Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe”

Mara tatu Yehova anawathibitisha waabudu wake washikamanifu kwamba atawasaidia.

Yeremia 29:11 Yafafanuliwa​—“Ninajua Mambo Niliyowapangia”

Je, Mungu ana mpango hususa kwa ajili ya kila mtu?

Yeremia 33:3 Yafafanuliwa​—“Niite, Nami Nitakuitikia”

Mungu aliahidi kuwafunulia “mambo makubwa na yasiyoeleweka” wale waliokubali mwaliko wake. Mambo gani? Je, mwaliko huo umetolewa leo pia?

Mika 6:8 Yafafanuliwa​—“Kwenda kwa Unyenyekevu na Mungu Wako”

Mstari huu unaonyesha kwa ufupi kwamba Mungu anatarajia mambo matatu muhimu kutoka kwetu.

Mathayo 6:33 Yafafanuliwa​—“Kuutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu”

Je, Yesu alimaanisha kwamba Wakristo hawahitaji kufanya kazi ili kupata riziki?

Mathayo 6:34 Yafafanuliwa​—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”

Yesu hakumaanisha kwamba tunapaswa kuepuka kupanga mambo ya wakati ujao.

Mathayo 11:28-30 Yafafanuliwa​—“Njoni Kwangu, . . . Nami Nitawapumzisha”

Je, Yesu aliahidi kwamba ukosefu wa haki na matatizo yote yangeisha mara moja?

Marko 1:15 Yafafanuliwa​—“Ufalme wa Mungu Umekaribia”

Je, Yesu alimaanisha kwamba tayari Ufalme ulikuwa umeanza kutawala?

Marko 11:24 Yafafanuliwa​—“Mnaposali na Kuomba Kitu, Aminini Kwamba Mmekipokea”

Ushauri wa Yesu kuhusu imani na sala unaweza kutusaidiaje kushinda changamoto leo?

Luka 1:37 Yafafanuliwa​—“Kwa Kuwa Hakuna Neno Lisilowezekana kwa Mungu”

Hakuna kinachoweza kumzuia Mungu Mweza-Yote kutimiza ahadi zake. Hilo linamaanisha nini kwako?

Yohana 1:1 Yafafanuliwa​—“Hapo Mwanzo Neno Alikuwako”

Andiko hili linazungumzia maisha ya Yesu Kristo kabla ya kuja duniani akiwa mwanadamu.

Yohana 3:16 Yafafanuliwa​—“Kwa Maana, Mungu Aliupenda Ulimwengu”

Yehova Mungu alionyeshaje kwamba anatupenda kila mmoja wetu na anataka tuishi milele?

Yohana 14:6 Yafafanuliwa​—“Mimi ndiye Njia na Kweli na Uzima”

Kwa nini mtu anayetaka kumwabudu Yehova anapaswa kutambua jukumu la pekee la Yesu?

Yohana 14:27 Yafafanuliwa​—“Amani Nawaachieni”

Yesu aliwapa au kuwaachia wafuasi wake waaminifu amani ya aina gani? Tunawezaje kuipata?

Yohana 15:13 Yafafanuliwa​—“Hakuna Upendo Mkuu Zaidi”

Wafuasi wa Yesu wanaweza kuigaje upendo ambao alionyesha?

Yohana 16:33 Yafafanuliwa​—“Mimi Nimeushinda Ulimwengu”

Maneno ya Yesu yanawahakikishiaje wafuasi wake kwamba wanaweza kufanikiwa kumpendeza Mungu?

Matendo 1:8 Yafafanuliwa​—“Mtapokea Nguvu”

Yesu aliwaahidi wafuasi wake nguvu gani, na nguvu hiyo ingewasaidia kufanya nini?

Waroma 5:8 Yafafanuliwa—“Kristo Alikufa kwa Ajili Yetu, Tulipokuwa Tungali Wenye Dhambi”

Kwa kuwa wanadamu wana mwelekeo wa kufikiri na kutenda kwa njia inayokiuka viwango vya uadilifu vya Mungu, tunawezaje kuwa na uhusiano mzuri na Mungu sasa na tarajio la kupata uzima wa milele wakati ujao?

Waroma 6:23 Yafafanuliwa​—“Mshahara wa Dhambi Ni Kifo; Lakini Zawadi Anayotoa Mungu Ni Uhai wa Milele”

Hakuna mwanadamu mwenye dhambi anayeweza kujipatia wokovu, lakini tunaweza kukubali zawadi ya Mungu ya uzima wa milele. Jinsi gani?

Waroma 10:13 Yafafanuliwa​—“Anayeliitia Jina la Bwana”

Mungu anawapa watu wa namna zote fursa ya kuokolewa na kupata uzima wa milele, bila kuzingatia taifa lao, rangi yao, au uwezo wao wa kifedha.

Waroma 12:12 Yafafanuliwa​—“Kwa Tumaini, Mkifurahi; Katika Dhiki, Mkisubiri; Katika Kusali, Mkidumu”

Wakristo wanawezaje kudumisha uaminifu wao licha ya mateso na matatizo mengine?

Waroma 15:13 Yafafanuliwa​—“Basi Mungu wa Tumaini na Awajaze Ninyi Furaha Yote na Amani”

Sifa ya shangwe na amani zinahusianaje na tumaini na roho takatifu?

1 Wakorintho 10:13 Yafafanuliwa​—“Mungu Ni Mwaminifu”

Ni katika njia zipi uaminifu wa Mungu unatusaidia hasa tunapokabili vishawishi?

2 Wakorintho 12:9 Yafafanuliwa​—“Neema Yangu Yakutosha”

Mtume Paulo alinufaika kwa njia kubwa kutokana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu? Sisi tunawezaje kunufaika nazo?

Wagalatia 6:9 Yafafanuliwa​—“Hivyo, Tusichoke Katika Kutenda Mema”

Wakristo wanaoendelea kufanya mema watapata thawabu gani?

Waefeso 3:20 Yafafanuliwa​—“[Mungu] Aweza Kufanya Mambo Makuu Zaidi ya Yale Tuwezayo Kuomba au Kufikiria”

Ni katika njia zipi Mungu anajibu sala na kutimiza matarajio ya waabudu wake?

Wafilipi 4:6, 7 Yafafanuliwa​—“Msihangaike Kuhusiana na Jambo Lolote”

Ni sala za aina gani zinazoweza kuwasaidia watumishi wa Mungu kupunguza mahangaiko na kuwa na amani ya moyoni?

Wafilipi 4:13 Yafafanuliwa​—“Ninaweza Kufanya Maneno Yote Katika Kristo”

Paulo alimaanisha nini alipoandika angepokea nguvu “kwa mambo yote”?

Wakolosai 3:23 Yafafanuliwa—“Lo Lote Mfanyalo, Lifanyeni kwa Moyo”

Mtazamo wa Mkristo kuhusu kazi unaweza kuwa na uvutano gani na uhusiano wake na Mungu?

2 Timotheo 1:7 Yafafanuliwa​—“Mungu Hakutupa Roho ya Woga”

Mungu anaweza kumsaidiaje mtu kushinda woga na kufanya yaliyo sawa kwa ujasiri?

Waebrania 4:12 Yafafanuliwa​—“Neno la Mungu Liko Hai na Linatenda Kazi”

Je, unaruhusu neno la Mungu litende kazi maishani mwako? Hilo linafunua nini kukuhusu?

Waebrania 11:1 Yafafanuliwa​—“Imani Ni Kuwa na Hakika ya Mambo Yatarajiwayo”

Imani halisi ina nguvu kadiri gani, nayo ni muhimu kiasi gani?

1 Petro 5:6, 7 Yafafanuliwa​—“Nyenyekeeni . . . Mkimtwika Yeye Fadhaa Zenu Zote”

Inamaanisha nini “kumtwika” Mungu mahangaiko yetu, na hilo linawezaje kutuletea kitulizo?

Ufunuo 21:1 Yafafanuliwa​—“ Mbingu Mpya na Dunia Mpya”

Biblia inatusaidiaje kuelewa maana ya mstari huu?