Hamia kwenye habari

Mikutano ya Kutaniko ya Mashahidi wa Yehova

Jifunze kuhusu mikutano yetu. Pata mikutano iliyo katika eneo lililo karibu nawe.

Pata Eneo Lililo Karibu Nawe (opens new window)

Ni Nini Hutukia Katika Mikutano Yetu?

Mashahidi wa Yehova huwa na mikutano ya ibada mara mbili kila juma. (Waebrania 10:24, 25) Katika mikutano hiyo, ambayo kila mtu anaalikwa, sisi huchunguza kile ambacho Biblia inasema na jinsi tunavyoweza kutumia mafundisho yake maishani mwetu.

Mikutano yetu mingi inatia ndani mazungumzo na wasikilizaji, ambayo ni kama tu mazungumzo ya darasani. Mikutano hufunguliwa na kufungwa kwa wimbo na sala.

Si lazima uwe Shahidi wa Yehova ili uhudhurie mikutano yetu. Tunakaribisha kila mtu. Hakuna malipo. Hakuna sadaka zinazokusanywa.