Hamia kwenye habari

Ukumbusho wa Kifo cha Yesu

Jumapili, Machi 24, 2024

Mashahidi wa Yehova huadhimisha ukumbusho wa kifo cha Yesu mara moja kila mwaka kama Yesu alivyoamuru aliposema: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”​—Luka 22:19.

Tunakukaribisha kuhudhuria tukio hili.

Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi

Programu hiyo itakuwa na urefu gani?

Ni programu ya saa moja hivi.

Programu hiyo itafanyika wapi?

Wasiliana na Mashahidi wa Yehova ili kujua inafanyika wapi katika eneo ulilopo.

Je, ninapaswa kulipa kiingilio?

Hapana.

Je, kuna michango itakayokusanywa?

Hapana. Mashahidi wa Yehova hawakusanyi michango katika mikutano yao kamwe.

Ninapaswa kuvalia jinsi gani?

Ingawa hutupangi mavazi maalum yanayopaswa kuvaliwa katika Ukumbusho, Mashahidi wa Yehova hujitahidi kufuata ushauri wa Biblia kuhusu kuvalia kwa kiasi na kwa heshima. (1 Timotheo 2:9) Huhitaji kuvalia mavazi ya gharama au yanayometa-meta.

Ni nini kitakachofanywa kwenye Ukumbusho huo?

Mkutano huo huanza na kumalizika kwa wimbo, na pia sala inatolewa na mhudumu wa Mashahidi wa Yehova. Sehemu kuu ya Ukumbusho ni hotuba inayozungumzia umuhimu wa kifo cha Yesu na jinsi tunavyonufaika kutokana na kile ambacho Mungu na Kristo wametufanyia.