Ukumbusho wa Kifo cha Yesu
Jumanne, Aprili 4, 2023
Mashahidi wa Yehova huadhimisha ukumbusho wa kifo cha Yesu mara moja kila mwaka kama Yesu alivyoamuru aliposema: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”—Luka 22:19.
Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi
Programu hiyo itakuwa na urefu gani?
Ni programu ya saa moja hivi.
Ni nini kitakachofanywa kwenye Ukumbusho huo?
Mkutano huo huanza na kumalizika kwa wimbo, na pia sala inayotolewa na mhudumu wa Mashahidi wa Yehova. Sehemu kuu ya Ukumbusho ni hotuba inayozungumzia umuhimu wa kifo cha Yesu na jinsi tunavyonufaika kutokana na kile ambacho Mungu na Kristo wametufanyia.
Kwa habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanaadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana kwa Njia Tofauti na Dini Nyingine?”