Ukumbusho wa Kifo cha Yesu
Jumatatu, Machi 22, 2027
Mara moja kila mwaka, Mashahidi wa Yehova huadhimisha kifo cha Yesu kama tu alivyoamuru aliposema: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”—Luka 22:19.
Tunakualika wewe na familia yako kuhudhuria tukio hili.
Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi
Ni nani anayeweza kuhudhuria?
Kila mtu anakaribishwa. Jihisi huru kuja pamoja na rafiki na familia yako.
Programu hiyo itachukua muda gani?
Ni programu ya saa moja hivi.
Programu hiyo itafanyika wapi?
Wasiliana na Mashahidi wa Yehova ili kujua itafanyika wapi katika eneo ulilopo.
Je, kuna malipo ya kiingilio au ada zozote?
Hapana.
Je, kuna sadaka zitakazokusanywa?
Hapana. Hatukusanyi sadaka katika mikutano yetu.—Mathayo 10:8.
Je, ninapaswa kuvaa mavazi hususa?
Hapana. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova hujitahidi kuvaa kwa njia ya heshima kwa ajili ya tukio hili muhimu.
Ni nini kitakachofanywa kwenye Ukumbusho huo?
Kutakuwa na hotuba yenye kutia moyo itakayozungumzia umuhimu wa kifo cha Yesu na jinsi tunavyonufaika kutokana na kile ambacho Mungu na Kristo wametufanyia. Programu hiyo itaanza na kumalizika kwa wimbo na sala.
Kwa habari zaidi, soma makala yenye kichwa “Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanaadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana kwa Njia Tofauti na Dini Nyingine?”
Ukumbusho wa mwaka wa 2027, 2028 na 2029 utafanywa tarehe gani?
2027: Jumatatu, Machi 22
2028: Jumapili, Aprili 9
2029: Alhamisi, Machi 29

