Zaburi 139:1-24
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+
2 Wewe mwenyewe umepata kujua kuketi kwangu na kusimama kwangu.+Umeichunguza fikira yangu tokea mbali.+
3 Umepima kusafiri kwangu na kulala kwangu nikiwa nimejinyoosha,+Nawe umezijua njia zangu zote.+
4 Kwa maana hamna neno hata moja katika ulimi wangu,+Lakini, tazama! Ee Yehova, tayari unajua yote.+
5 Nyuma na mbele umenizingira;Nawe unauweka mkono wako juu yangu.
6 Ujuzi wa namna hiyo ni wa ajabu mno kwangu.+Ni wa juu sana hivi kwamba siwezi kuufikia.+
7 Ni wapi ninapoweza kwenda mbali na roho yako,+Na ni wapi ninapoweza kukimbilia mbali na uso wako?+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko;+Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* tazama! ungekuwa huko.+
9 Kama ningechukua mabawa+ ya mapambazuko,Ili nipate kuishi katika bahari ya mbali sana,+
10 Huko, pia, mkono wako ungeniongoza+Nao mkono wako wa kuume ungenishika.+
11 Na kama ningesema: “Hakika giza litanifunika haraka!”+Ndipo usiku ungekuwa nuru kunizunguka.+
12 Hata giza lenyewe halingekuwa jeusi mno kwako,+Lakini usiku wenyewe ungeng’aa kama mchana;+Giza lingekuwa sawa tu na nuru.+
13 Kwa maana wewe mwenyewe uliumba figo zangu;+Wewe uliniweka nikiwa nimekingwa katika tumbo la mama yangu.+
14 Nitakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.+Kazi zako ni za ajabu,+Kama vile nafsi yangu inavyojua vema.+
15 Mifupa yangu haikufichwa kwako+Nilipofanyizwa katika siri,+Nilipoungwa katika sehemu za chini kabisa+ za dunia.
16 Macho yako yalikiona kiini-tete changu,+Na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa,Kuhusiana na siku ambazo zilifanyizwa+Na hakukuwako hata moja kati ya hizo.
17 Kwa hiyo, jinsi mawazo yako yalivyo yenye thamani kwangu!+Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kuu!+
18 Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za mchanga.+Nimeamka, na bado niko pamoja nawe.+
19 Laiti wewe, Ee Mungu, ungemuua mwovu!+Ndipo hata watu wenye hatia ya damu+ hakika wangeniondokea,
20 Wanaosema mambo juu yako kulingana na wazo lao;+Wamelitumia jina lako vibaya+—wapinzani wako.+
21 Je, mimi siwachukii wale wanaokuchukia vikali, Ee Yehova,+Na je, sichukizwi na wale wanaokuasi?+
22 Kwa chuki kamili, ninawachukia.+Wamekuwa adui halisi kwangu.+
23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha,+
24 Na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza,+Na uniongoze katika njia+ ya mpaka wakati usio na kipimo.
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.