Zaburi 7:1-17

Wimbo wa huzuni wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini. 7  Ee Yehova Mungu wangu,+ nimekukimbilia wewe.+Uniokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unikomboe,+   Ili mtu yeyote asiirarue nafsi yangu vipande-vipande kama simba anavyofanya,+Kuninyakua wakati ambapo hakuna mkombozi.+   Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimefanya hili,+Ikiwa kuna ukosefu wowote wa haki katika mikono yangu,+   Ikiwa nimemlipa ubaya yule anayenipa thawabu,+Au ikiwa nimempora yeyote anayenionyesha uadui bila kufanikiwa,+   Adui na aifuatilie nafsi yangu+Naye afikie na kukanyagia chini uhai wanguNa kufanya utukufu wangu ukae mavumbini. Sela.   Usimame, Ee Yehova, katika hasira yako;+Uinuke katika milipuko ya ghadhabu ya wale wanaonionyesha uadui,+Na uamke kwa ajili yangu,+ kwa maana umetoa amri kwa ajili ya hukumu.+   Nalo kusanyiko la vikundi vya mataifa na likuzunguke,Nawe urudi juu dhidi yake.   Yehova mwenyewe atavihukumu vikundi vya watu.+Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu+Na kulingana na utimilifu+ wangu ulio ndani yangu.   Tafadhali, ubaya wa waovu na ufikie mwisho,+Nawe umwimarishe mwadilifu;+Na Mungu akiwa mwadilifu+ anapima moyo+ na figo.+ 10  Ngao yangu iko juu ya Mungu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+ 11  Mungu ni Mwamuzi mwadilifu,+Na Mungu anazitupa shutuma kila siku. 12  Ikiwa mtu yeyote hatarudi,+ Yeye ataunoa upanga wake,+Hakika ataupinda upinde wake, naye atauweka tayari ili kufyatuliwa.+ 13  Naye atajitayarishia silaha za kifo;+Mishale yake ataifanya kuwa yenye kuwaka moto.+ 14  Tazama! Kuna mtu aliye na mimba ya jambo lenye kuumiza,+Naye amechukua mimba ya taabu na hatakosa kuzaa uwongo.+ 15  Amechimbua shimo, naye akalichimba;+Lakini ataanguka katika shimo alilolifanyiza.+ 16  Taabu yake itarudi juu ya kichwa chake mwenyewe,+Na jeuri yake mwenyewe itashuka juu ya utosi wa kichwa chake.+ 17  Nitamsifu Yehova kulingana na uadilifu wake,+Nami nitalipigia muziki jina+ la Yehova Aliye Juu Zaidi.+

Maelezo ya Chini