Zaburi 7:1-17
Wimbo wa huzuni wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini.
7 Ee Yehova Mungu wangu,+ nimekukimbilia wewe.+Uniokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unikomboe,+
2 Ili mtu yeyote asiirarue nafsi yangu vipande-vipande kama simba anavyofanya,+Kuninyakua wakati ambapo hakuna mkombozi.+
3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimefanya hili,+Ikiwa kuna ukosefu wowote wa haki katika mikono yangu,+
4 Ikiwa nimemlipa ubaya yule anayenipa thawabu,+Au ikiwa nimempora yeyote anayenionyesha uadui bila kufanikiwa,+
5 Adui na aifuatilie nafsi yangu+Naye afikie na kukanyagia chini uhai wanguNa kufanya utukufu wangu ukae mavumbini. Sela.
6 Usimame, Ee Yehova, katika hasira yako;+Uinuke katika milipuko ya ghadhabu ya wale wanaonionyesha uadui,+Na uamke kwa ajili yangu,+ kwa maana umetoa amri kwa ajili ya hukumu.+
7 Nalo kusanyiko la vikundi vya mataifa na likuzunguke,Nawe urudi juu dhidi yake.
8 Yehova mwenyewe atavihukumu vikundi vya watu.+Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu+Na kulingana na utimilifu+ wangu ulio ndani yangu.
9 Tafadhali, ubaya wa waovu na ufikie mwisho,+Nawe umwimarishe mwadilifu;+Na Mungu akiwa mwadilifu+ anapima moyo+ na figo.+
10 Ngao yangu iko juu ya Mungu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+
11 Mungu ni Mwamuzi mwadilifu,+Na Mungu anazitupa shutuma kila siku.
12 Ikiwa mtu yeyote hatarudi,+ Yeye ataunoa upanga wake,+Hakika ataupinda upinde wake, naye atauweka tayari ili kufyatuliwa.+
13 Naye atajitayarishia silaha za kifo;+Mishale yake ataifanya kuwa yenye kuwaka moto.+
14 Tazama! Kuna mtu aliye na mimba ya jambo lenye kuumiza,+Naye amechukua mimba ya taabu na hatakosa kuzaa uwongo.+
15 Amechimbua shimo, naye akalichimba;+Lakini ataanguka katika shimo alilolifanyiza.+
16 Taabu yake itarudi juu ya kichwa chake mwenyewe,+Na jeuri yake mwenyewe itashuka juu ya utosi wa kichwa chake.+
17 Nitamsifu Yehova kulingana na uadilifu wake,+Nami nitalipigia muziki jina+ la Yehova Aliye Juu Zaidi.+