Zaburi 30:1-12
Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba.+ Wa Daudi.
30 Nitakutukuza wewe, Ee Yehova, kwa maana umeniinua+Nawe hukuwaruhusu adui zangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+
3 Ee Yehova, umeitoa nafsi yangu kutoka katika Kaburi;*+Umeendelea kuniweka nikiwa hai, ili nisipate kushuka ndani ya shimo.+
4 Mpigieni Yehova muziki, enyi washikamanifu wake,+Utoleeni shukrani ukumbusho wake mtakatifu;+
5 Kwa sababu kuwa chini ya hasira yake ni kwa muda kidogo tu,+Kuwa chini ya nia yake njema ni kwa muda wote wa maisha.+Huenda kilio kikakaa wakati wa jioni,+ lakini asubuhi kuna vigelegele vya shangwe.+
6 Mimi nimesema katika starehe yangu:+“Sitatikiswa kamwe.”+
7 Ee Yehova, umeusimamisha mlima wangu katika nguvu kwa nia yako njema.+Uliuficha uso wako; nikawa na wasiwasi.+
8 Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+Nami niliendelea kumsihi Yehova anipe kibali.+
9 Damu yangu ina faida gani ninaposhuka katika shimo?+Je, mavumbi yatakusifu wewe?+ Je, yatasema juu ya ukweli wako?+
10 Usikie, Ee Yehova, na kunionyesha kibali.+Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+
11 Umenibadilishia maombolezo yangu yakawa kucheza dansi;+Umefungua nguo yangu ya gunia, nawe unaendelea kunifunga shangwe,+
12 Ili utukufu wangu upate kukupigia muziki wala usinyamaze.+Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo.+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.