Zaburi 30:1-12

Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba.+ Wa Daudi. 30  Nitakutukuza wewe, Ee Yehova, kwa maana umeniinua+Nawe hukuwaruhusu adui zangu washangilie juu yangu.+   Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+   Ee Yehova, umeitoa nafsi yangu kutoka katika Kaburi;*+Umeendelea kuniweka nikiwa hai, ili nisipate kushuka ndani ya shimo.+   Mpigieni Yehova muziki, enyi washikamanifu wake,+Utoleeni shukrani ukumbusho wake mtakatifu;+   Kwa sababu kuwa chini ya hasira yake ni kwa muda kidogo tu,+Kuwa chini ya nia yake njema ni kwa muda wote wa maisha.+Huenda kilio kikakaa wakati wa jioni,+ lakini asubuhi kuna vigelegele vya shangwe.+   Mimi nimesema katika starehe yangu:+“Sitatikiswa kamwe.”+   Ee Yehova, umeusimamisha mlima wangu katika nguvu kwa nia yako njema.+Uliuficha uso wako; nikawa na wasiwasi.+   Niliendelea kukuita, Ee Yehova;+Nami niliendelea kumsihi Yehova anipe kibali.+   Damu yangu ina faida gani ninaposhuka katika shimo?+Je, mavumbi yatakusifu wewe?+ Je, yatasema juu ya ukweli wako?+ 10  Usikie, Ee Yehova, na kunionyesha kibali.+Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+ 11  Umenibadilishia maombolezo yangu yakawa kucheza dansi;+Umefungua nguo yangu ya gunia, nawe unaendelea kunifunga shangwe,+ 12  Ili utukufu wangu upate kukupigia muziki wala usinyamaze.+Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu mpaka wakati usio na kipimo.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.