Zaburi 63:1-11

Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+ 63  Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+Nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako.+Mwili wangu umezimia kwa kukutamani wewe.Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.+   Hivyo nimekuona katika mahali patakatifu,+Kwa kuona nguvu zako na utukufu wako.+   Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni bora kuliko uzima,+Midomo yangu mwenyewe itakusifu.+   Kwa hiyo nitakusifu muda wote wa maisha yangu;+Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.+   Nafsi yangu imeshiba sehemu bora, naam, mafuta,+Na kwa midomo yenye vigelegele vya shangwe kinywa changu hutoa sifa.+   Wakati ninapokukumbuka kitandani mwangu,+Wakati wa makesha ya usiku natafakari juu yako.+   Kwa maana umenisaidia,+Na katika kivuli cha mabawa yako napiga vigelegele kwa shangwe.+   Nafsi yangu imekufuata karibu-karibu;+Mkono wako wa kuume unanishika sana.+   Nao wale wanaoendelea kuitafuta nafsi yangu ili waiharibu,+Wataingia katika sehemu za chini kabisa za dunia.+ 10  Watatiwa katika nguvu za upanga;+Watakuwa fungu la mbweha.+ 11  Naye mfalme mwenyewe atashangilia katika Mungu.+Kila anayeapa kwa jina lake atajisifu,+Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitazibwa.+

Maelezo ya Chini