Zaburi 63:1-11
Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+Nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako.+Mwili wangu umezimia kwa kukutamani wewe.Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.+
2 Hivyo nimekuona katika mahali patakatifu,+Kwa kuona nguvu zako na utukufu wako.+
3 Kwa sababu fadhili zako zenye upendo ni bora kuliko uzima,+Midomo yangu mwenyewe itakusifu.+
4 Kwa hiyo nitakusifu muda wote wa maisha yangu;+Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.+
5 Nafsi yangu imeshiba sehemu bora, naam, mafuta,+Na kwa midomo yenye vigelegele vya shangwe kinywa changu hutoa sifa.+
6 Wakati ninapokukumbuka kitandani mwangu,+Wakati wa makesha ya usiku natafakari juu yako.+
7 Kwa maana umenisaidia,+Na katika kivuli cha mabawa yako napiga vigelegele kwa shangwe.+
8 Nafsi yangu imekufuata karibu-karibu;+Mkono wako wa kuume unanishika sana.+
9 Nao wale wanaoendelea kuitafuta nafsi yangu ili waiharibu,+Wataingia katika sehemu za chini kabisa za dunia.+
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;+Watakuwa fungu la mbweha.+
11 Naye mfalme mwenyewe atashangilia katika Mungu.+Kila anayeapa kwa jina lake atajisifu,+Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitazibwa.+