Zaburi 103:1-22
Ya Daudi.
103 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,+Naam, kila kitu kilicho ndani yangu, na kilibariki jina lake takatifu.+
2 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,Wala usiyasahau matendo yake yote,+
3 Yeye anayesamehe makosa yako yote,+Anayeponya magonjwa yako yote,+
4 Anayeuokoa uhai wako kutoka katika shimo,+Anayekuvika taji la fadhili zenye upendo na rehema,+
5 Anayeushibisha muda wote wa maisha yako kwa mambo mema;+Ujana wako unajifanya upya kama ule wa tai.+
6 Yehova anatekeleza matendo ya uadilifu+Na hukumu kwa wale wote wanaopunjwa.+
7 Alimjulisha Musa njia zake,+Matendo yake kwa wana wa Israeli.+
8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+
9 Yeye hataendelea kutafuta makosa wakati wote,+Wala hataendelea kuweka kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+
10 Hakututendea kulingana na dhambi zetu;+Wala kuleta juu yetu kile tunachostahili kulingana na makosa yetu.+
11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+Ndivyo fadhili zake zenye upendo zilivyo kuu kuwaelekea wale wanaomwogopa.+
12 Kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,+Ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+
14 Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu,+Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.+
15 Naye mwanadamu anayeweza kufa, siku zake ni kama zile za majani mabichi;+Yeye huchanuka kama ua la shambani.+
16 Kwa maana upepo unapita juu yake, nalo halipo tena;+Napo mahali pake hapataendelea kulitambua tena.+
17 Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+
18 Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+
19 Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni;+Nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.+
20 Mbarikini Yehova, enyi malaika zake,+ mlio na uwezo katika nguvu, mnaolitenda neno lake,+Kwa kuisikiliza sauti ya neno lake.+
21 Mbarikini Yehova, enyi majeshi yake yote,+Enyi wahudumu wake, mnaofanya mapenzi yake.+
22 Mbarikini Yehova, enyi kazi zake zote,+Katika mahali pote pa utawala wake.+Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+