Zaburi 103:1-22

Ya Daudi. 103  Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,+Naam, kila kitu kilicho ndani yangu, na kilibariki jina lake takatifu.+   Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,Wala usiyasahau matendo yake yote,+   Yeye anayesamehe makosa yako yote,+Anayeponya magonjwa yako yote,+   Anayeuokoa uhai wako kutoka katika shimo,+Anayekuvika taji la fadhili zenye upendo na rehema,+   Anayeushibisha muda wote wa maisha yako kwa mambo mema;+Ujana wako unajifanya upya kama ule wa tai.+   Yehova anatekeleza matendo ya uadilifu+Na hukumu kwa wale wote wanaopunjwa.+   Alimjulisha Musa njia zake,+Matendo yake kwa wana wa Israeli.+   Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+   Yeye hataendelea kutafuta makosa wakati wote,+Wala hataendelea kuweka kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+ 10  Hakututendea kulingana na dhambi zetu;+Wala kuleta juu yetu kile tunachostahili kulingana na makosa yetu.+ 11  Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+Ndivyo fadhili zake zenye upendo zilivyo kuu kuwaelekea wale wanaomwogopa.+ 12  Kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,+Ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.+ 13  Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+ 14  Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu,+Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.+ 15  Naye mwanadamu anayeweza kufa, siku zake ni kama zile za majani mabichi;+Yeye huchanuka kama ua la shambani.+ 16  Kwa maana upepo unapita juu yake, nalo halipo tena;+Napo mahali pake hapataendelea kulitambua tena.+ 17  Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+ 18  Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+ 19  Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni;+Nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.+ 20  Mbarikini Yehova, enyi malaika zake,+ mlio na uwezo katika nguvu, mnaolitenda neno lake,+Kwa kuisikiliza sauti ya neno lake.+ 21  Mbarikini Yehova, enyi majeshi yake yote,+Enyi wahudumu wake, mnaofanya mapenzi yake.+ 22  Mbarikini Yehova, enyi kazi zake zote,+Katika mahali pote pa utawala wake.+Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+

Maelezo ya Chini