Zaburi 132:1-18

Wimbo wa Mipando. 132  Ukumbuke, Ee Yehova, juu ya Daudi+Fedheha zake zote;+   Jinsi alivyomwapia Yehova,+Jinsi alivyomwekea nadhiri Mwenye Nguvu+ wa Yakobo:+   “Sitaenda katika hema la nyumba yangu.+Sitapanda katika kitanda changu cha fahari,+   Sitaacha macho yangu kulala usingizi,+Wala macho yangu yenye kung’aa kusinzia,+   Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,+Maskani kuu kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+   Tazama! Tumeyasikia hayo huko Efratha,+Tumeyapata katika viwanja vya msitu.+   Na tuingie katika maskani yake kuu;+Na tuiname kwenye kiti chake cha miguu.+   Usimame, Ee Yehova, uende katika mahali pako pa kupumzika,+Wewe na Sanduku+ la nguvu zako.+   Makuhani wako na wavikwe uadilifu,+Nao washikamanifu wako na wapige vigelegele kwa shangwe.+ 10  Kwa sababu ya Daudi mtumishi wako,+Usiugeuze nyuma uso wa mtiwa-mafuta wako.+ 11  Yehova amemwapia Daudi,+Kwa kweli hataliacha:+“Kati ya uzao wa tumbo lako+Nitaweka juu ya kiti chako cha ufalme.+ 12  Ikiwa wana wako watalishika agano langu+Na vikumbusho vyangu ambavyo nitawafundisha,+Wana wao pia milele+Wataketi juu ya kiti chako cha ufalme.”+ 13  Kwa maana Yehova amechagua Sayuni;+Amepatamani pawe makao kwa ajili yake mwenyewe:+ 14  “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzika milele;+Nitakaa hapa, kwa maana nimepatamani.+ 15  Bila shaka nitavibariki vyakula vyake.+Maskini wake nitawashibisha kwa mkate.+ 16  Na makuhani wake nitawavika wokovu;+Na bila shaka washikamanifu wake watapiga vigelegele kwa shangwe. 17  Hapo nitaifanya pembe ya Daudi ikue.+Nimetayarisha taa kwa ajili ya mtiwa-mafuta wangu.+ 18  Adui zake nitawavika aibu;+Lakini taji+ lake litasitawi juu yake.”+

Maelezo ya Chini