Zaburi 132:1-18
Wimbo wa Mipando.
132 Ukumbuke, Ee Yehova, juu ya Daudi+Fedheha zake zote;+
2 Jinsi alivyomwapia Yehova,+Jinsi alivyomwekea nadhiri Mwenye Nguvu+ wa Yakobo:+
3 “Sitaenda katika hema la nyumba yangu.+Sitapanda katika kitanda changu cha fahari,+
4 Sitaacha macho yangu kulala usingizi,+Wala macho yangu yenye kung’aa kusinzia,+
5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,+Maskani kuu kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+
6 Tazama! Tumeyasikia hayo huko Efratha,+Tumeyapata katika viwanja vya msitu.+
7 Na tuingie katika maskani yake kuu;+Na tuiname kwenye kiti chake cha miguu.+
8 Usimame, Ee Yehova, uende katika mahali pako pa kupumzika,+Wewe na Sanduku+ la nguvu zako.+
9 Makuhani wako na wavikwe uadilifu,+Nao washikamanifu wako na wapige vigelegele kwa shangwe.+
10 Kwa sababu ya Daudi mtumishi wako,+Usiugeuze nyuma uso wa mtiwa-mafuta wako.+
11 Yehova amemwapia Daudi,+Kwa kweli hataliacha:+“Kati ya uzao wa tumbo lako+Nitaweka juu ya kiti chako cha ufalme.+
12 Ikiwa wana wako watalishika agano langu+Na vikumbusho vyangu ambavyo nitawafundisha,+Wana wao pia milele+Wataketi juu ya kiti chako cha ufalme.”+
13 Kwa maana Yehova amechagua Sayuni;+Amepatamani pawe makao kwa ajili yake mwenyewe:+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzika milele;+Nitakaa hapa, kwa maana nimepatamani.+
15 Bila shaka nitavibariki vyakula vyake.+Maskini wake nitawashibisha kwa mkate.+
16 Na makuhani wake nitawavika wokovu;+Na bila shaka washikamanifu wake watapiga vigelegele kwa shangwe.
17 Hapo nitaifanya pembe ya Daudi ikue.+Nimetayarisha taa kwa ajili ya mtiwa-mafuta wangu.+
18 Adui zake nitawavika aibu;+Lakini taji+ lake litasitawi juu yake.”+