Zaburi 148:1-14
148 Msifuni Yah!+Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+Msifuni katika vilele.+
2 Msifuni, enyi malaika zake wote.+Msifuni, enyi jeshi lake lote.+
3 Msifuni, enyi jua na mwezi.+Msifuni, enyi nyota zote za nuru.+
4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,+Nanyi maji yaliyo juu ya mbingu.+
5 Na vilisifu jina la Yehova;+Kwa maana yeye mwenyewe aliamuru, navyo vikaumbwa.+
6 Naye huendelea kuvisimamisha milele, mpaka wakati usio na kipimo.+Amelitoa sharti, nalo halitapitilia mbali.+
7 Msifuni Yehova kutoka duniani,+Enyi wanyama wakubwa wa baharini, nanyi vilindi vyote vya maji,+
8 Enyi moto na mvua ya mawe, theluji na moshi mzito,+Enyi pepo zenye tufani, zinazotimiza neno lake,+
9 Enyi milima, nanyi vilima vyote,+Enyi miti ya matunda, nanyi mierezi yote,+
10 Enyi wanyama wa mwitu, nanyi wanyama wote wa kufugwa,+Enyi vitu vinavyotambaa na ndege wenye mabawa,+
11 Enyi wafalme wa dunia,+ nanyi vikundi vyote vya mataifa,Enyi wakuu,+ nanyi waamuzi wa dunia,+
12 Enyi vijana,+ nanyi mabikira pia,+Enyi wazee+ pamoja na wavulana.+
13 Na walisifu jina la Yehova,+Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+Utukufu wake uko juu ya dunia na mbingu.+
14 Naye ataiinua pembe ya watu wake,+Sifa ya washikamanifu wake wote,+Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.+Msifuni Yah!+