Zaburi 148:1-14

148  Msifuni Yah!+Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+Msifuni katika vilele.+   Msifuni, enyi malaika zake wote.+Msifuni, enyi jeshi lake lote.+   Msifuni, enyi jua na mwezi.+Msifuni, enyi nyota zote za nuru.+   Msifuni, enyi mbingu za mbingu,+Nanyi maji yaliyo juu ya mbingu.+   Na vilisifu jina la Yehova;+Kwa maana yeye mwenyewe aliamuru, navyo vikaumbwa.+   Naye huendelea kuvisimamisha milele, mpaka wakati usio na kipimo.+Amelitoa sharti, nalo halitapitilia mbali.+   Msifuni Yehova kutoka duniani,+Enyi wanyama wakubwa wa baharini, nanyi vilindi vyote vya maji,+   Enyi moto na mvua ya mawe, theluji na moshi mzito,+Enyi pepo zenye tufani, zinazotimiza neno lake,+   Enyi milima, nanyi vilima vyote,+Enyi miti ya matunda, nanyi mierezi yote,+ 10  Enyi wanyama wa mwitu, nanyi wanyama wote wa kufugwa,+Enyi vitu vinavyotambaa na ndege wenye mabawa,+ 11  Enyi wafalme wa dunia,+ nanyi vikundi vyote vya mataifa,Enyi wakuu,+ nanyi waamuzi wa dunia,+ 12  Enyi vijana,+ nanyi mabikira pia,+Enyi wazee+ pamoja na wavulana.+ 13  Na walisifu jina la Yehova,+Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+Utukufu wake uko juu ya dunia na mbingu.+ 14  Naye ataiinua pembe ya watu wake,+Sifa ya washikamanifu wake wote,+Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.+Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini