Zaburi 65:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.
65 Kwa ajili yako kuna sifa—kimya—, Ee Mungu, katika Sayuni;+Na kwako wewe nadhiri itatimizwa.+
2 Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.+
3 Mambo yenye makosa yamekuwa na nguvu kuliko mimi.+Nayo makosa yetu, wewe mwenyewe utayafunika.+
4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumfanya akaribie,+Ili apate kukaa katika nyua zako.+Hakika tutashiba mema ya nyumba yako,+Mahali patakatifu pa hekalu lako.+
5 Utatujibu kwa mambo yenye kuogopesha katika uadilifu,+Ee Mungu wa wokovu wetu,+Tegemeo la mipaka yote ya dunia na wale walio mbali baharini.+
6 Anaifanya imara milima kwa nguvu zake;+Kwa kweli yeye amefungwa mshipi wa nguvu.+
7 Anatuliza kelele za bahari,+Kelele za mawimbi yake na ghasia za vikundi vya mataifa.+
8 Na wakaaji wa sehemu za mbali zaidi wataogopa ishara zako;+Unafanya kutokea kwa asubuhi na jioni kupige vigelegele kwa shangwe.+
9 Umeielekezea dunia fikira zako, ili uipatie wingi;+Unaitajirisha sana.Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji.+Wewe unatayarisha nafaka yao,+Kwa maana hivyo ndivyo unavyoitayarisha dunia.+
10 Mitaro yake inajazwa maji, madonge yake yanasawazishwa;+Unailainisha kwa manyunyu mengi; unaibariki mimea yake.+
11 Umeuvika taji mwaka kwa wema wako,+Nayo mapito yako yanadondoka mafuta.+
12 Viwanja vya malisho ya nyikani vinaendelea kudondoka mafuta,+Navyo vilima vinajifunga shangwe kama mshipi.+
13 Malisho yamevikwa makundi,+Na nchi tambarare za chini zimefunikwa na nafaka.+Vitu hivyo vinapiga kelele za ushindi, naam, vinaimba.+