Zaburi 65:1-13

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo. 65  Kwa ajili yako kuna sifa—kimya—, Ee Mungu, katika Sayuni;+Na kwako wewe nadhiri itatimizwa.+   Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.+   Mambo yenye makosa yamekuwa na nguvu kuliko mimi.+Nayo makosa yetu, wewe mwenyewe utayafunika.+   Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumfanya akaribie,+Ili apate kukaa katika nyua zako.+Hakika tutashiba mema ya nyumba yako,+Mahali patakatifu pa hekalu lako.+   Utatujibu kwa mambo yenye kuogopesha katika uadilifu,+Ee Mungu wa wokovu wetu,+Tegemeo la mipaka yote ya dunia na wale walio mbali baharini.+   Anaifanya imara milima kwa nguvu zake;+Kwa kweli yeye amefungwa mshipi wa nguvu.+   Anatuliza kelele za bahari,+Kelele za mawimbi yake na ghasia za vikundi vya mataifa.+   Na wakaaji wa sehemu za mbali zaidi wataogopa ishara zako;+Unafanya kutokea kwa asubuhi na jioni kupige vigelegele kwa shangwe.+   Umeielekezea dunia fikira zako, ili uipatie wingi;+Unaitajirisha sana.Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji.+Wewe unatayarisha nafaka yao,+Kwa maana hivyo ndivyo unavyoitayarisha dunia.+ 10  Mitaro yake inajazwa maji, madonge yake yanasawazishwa;+Unailainisha kwa manyunyu mengi; unaibariki mimea yake.+ 11  Umeuvika taji mwaka kwa wema wako,+Nayo mapito yako yanadondoka mafuta.+ 12  Viwanja vya malisho ya nyikani vinaendelea kudondoka mafuta,+Navyo vilima vinajifunga shangwe kama mshipi.+ 13  Malisho yamevikwa makundi,+Na nchi tambarare za chini zimefunikwa na nafaka.+Vitu hivyo vinapiga kelele za ushindi, naam, vinaimba.+

Maelezo ya Chini