Zaburi 95:1-11
95 Njooni tumpigie Yehova vigelegele kwa shangwe!+Na tumpigie Mwamba wetu wa wokovu vigelegele vya ushindi.+
2 Twendeni mbele za uso wake tukiwa na shukrani;+Na tumpigie kelele za ushindi kwa nyimbo tamu.+
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu+Na Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote,+
4 Yeye ambaye mkononi mwake mna vina vya ndani sana vya dunia+Na ambaye vilele vya milima ni vyake;+
5 Ambaye bahari, aliyoiumba yeye mwenyewe, ni yake+Na ambaye mikono yake mwenyewe iliifanyiza nchi kavu.+
6 Ingieni, tuabudu na kuinama;+Na tupige magoti+ mbele za Yehova Mtengenezaji wetu.+
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake.+Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+
8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama huko Meriba,+Kama katika ile siku ya Masa, nyikani,+
9 Wakati mababu zenu waliponijaribu;+Walinichunguza, pia waliuona utendaji wangu.+
10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho,+Nami nikasema:“Wao ni kikundi cha watu waliopotoka moyoni,+Nao wenyewe hawajapata kuzijua njia zangu”;+
11 Ambao niliapa juu yao kwa hasira yangu:+“Hawataingia katika mahali pangu pa kupumzikia.”+