Zaburi 27:1-14

Ya Daudi. 27  Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.+ Nitamwogopa nani?+Yehova ni ngome ya uhai wangu.+Nitamhofu nani?+   Watenda-maovu walipokuja karibu juuyangu ili wapate kuila nyama yangu,+Wao wakiwa ni wapinzani wangu na adui zangu,+Wao walijikwaa na kuanguka.+   Hata kambi ijapopiga hema dhidi yangu,+Moyo wangu hautaogopa.+Vita vijapozuka dhidi yangu,+Bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.+   Nimemwomba Yehova jambo moja+Ndilo nitakalolitafuta,+Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+Ili kuuona uzuri wa Yehova+Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+   Kwa maana atanificha mafichoni mwake katika siku ya msiba;+Atanificha katika mahali pa siri pa hema lake;+Ataniweka juu kwenye mwamba.+   Na sasa kichwa changu kitakuwa juu, juu ya adui zangu wanaonizunguka pande zote;+Nami nitatoa kwenye hema lake dhabihu za vigelegele vya shangwe;+Nitamwimbia Yehova na kumpigia muziki.+   Usikie, Ee Yehova, ninapoita kwa sauti yangu,+Na unionyeshe kibali na kunijibu.+   Moyo wangu umesema hivi juu yako: “Utafuteni uso wangu.”+Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+   Usinifiche uso wako.+Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+Uwe msaada wangu.+Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+ 10  Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha,+Yehova mwenyewe angenichukua.+ 11  Unifundishe njia yako, Ee Yehova,+Na uniongoze katika njia ya unyoofu kwa sababu ya adui zangu. 12  Usinitie mikononi mwa nafsi ya wapinzani wangu;+Kwa maana dhidi yangu wamesimama mashahidi wa uwongo,+Na yeye anayetokeza jeuri.+ 13  Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai+—! 14  Mtumaini Yehova;+ uwe hodari na moyo wako uwe na nguvu.+Naam, mtumaini Yehova.+

Maelezo ya Chini