Zaburi 27:1-14
Ya Daudi.
27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.+
Nitamwogopa nani?+Yehova ni ngome ya uhai wangu.+Nitamhofu nani?+
2 Watenda-maovu walipokuja karibu juuyangu ili wapate kuila nyama yangu,+Wao wakiwa ni wapinzani wangu na adui zangu,+Wao walijikwaa na kuanguka.+
3 Hata kambi ijapopiga hema dhidi yangu,+Moyo wangu hautaogopa.+Vita vijapozuka dhidi yangu,+Bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.+
4 Nimemwomba Yehova jambo moja+—Ndilo nitakalolitafuta,+Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+Ili kuuona uzuri wa Yehova+Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+
5 Kwa maana atanificha mafichoni mwake katika siku ya msiba;+Atanificha katika mahali pa siri pa hema lake;+Ataniweka juu kwenye mwamba.+
6 Na sasa kichwa changu kitakuwa juu, juu ya adui zangu wanaonizunguka pande zote;+Nami nitatoa kwenye hema lake dhabihu za vigelegele vya shangwe;+Nitamwimbia Yehova na kumpigia muziki.+
7 Usikie, Ee Yehova, ninapoita kwa sauti yangu,+Na unionyeshe kibali na kunijibu.+
8 Moyo wangu umesema hivi juu yako: “Utafuteni uso wangu.”+Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+
9 Usinifiche uso wako.+Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+Uwe msaada wangu.+Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+
10 Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha,+Yehova mwenyewe angenichukua.+
11 Unifundishe njia yako, Ee Yehova,+Na uniongoze katika njia ya unyoofu kwa sababu ya adui zangu.
12 Usinitie mikononi mwa nafsi ya wapinzani wangu;+Kwa maana dhidi yangu wamesimama mashahidi wa uwongo,+Na yeye anayetokeza jeuri.+
13 Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai+—!
14 Mtumaini Yehova;+ uwe hodari na moyo wako uwe na nguvu.+Naam, mtumaini Yehova.+