Zaburi 104:1-35

104  Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+Ee Yehova Mungu wangu, umekuwa mkuu sana.+Umevaa utukufu na fahari,+   Unayejifunika nuru kama vazi,+Unayezitandaza mbingu kama hema,+   Yule anayejenga vyumba vyake vya juu kwa boriti katika maji,+Anayefanya mawingu kuwa gari lake,+Anayetembea juu ya mabawa ya upepo,+   Anayewafanya malaika zake kuwa roho,+Na wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza.+   Ameiwekea dunia msingi juu ya mahali pake palipofanywa imara;+Haitatikiswa mpaka wakati usio na kipimo, au milele.+   Uliifunika kwa kilindi cha maji kama kwa vazi.+Maji yalikuwa yamesimama juu ya milima.+   Yakaanza kukimbia ulipoyakemea;+Yakakimbia kwa wasiwasi mkubwa yaliposikia sauti ya mngurumo wako—   Milima ikapanda juu,+Nchi tambarare za mabonde zikashuka chini—Mpaka mahali ulipoyawekea msingi wake.   Uliweka mpaka, yasiupite,+Ili yasiifunike dunia tena.+ 10  Anatuma mabubujiko ndani ya mabonde yenye vijito;+Yanaendelea kusonga mbele katikati ya milima. 11  Daima yanawapa maji ya kunywa wanyama wote wa porini;+Punda-milia+ hukata kiu yao kwa ukawaida. 12  Juu yake hukaa viumbe vinavyoruka vya mbinguni;+Kutoka katikati ya majani mengi yanaendelea kuvuma.+ 13  Anainywesha maji milima kutoka katika vyumba vyake vya juu.+Dunia imeshiba matunda ya kazi zako.+ 14  Anafanya majani mabichi yachipuke kwa ajili ya wanyama,+Na mimea ili itumikie wanadamu,+Ili chakula kitokezwe duniani,+ 15  Na divai ambayo hufanya moyo wa mwanadamu anayeweza kufa ushangilie,+Kuufanya uso ung’ae kwa mafuta,+Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+ 16  Miti ya Yehova imeshiba,Mierezi ya Lebanoni ambayo aliipanda.+ 17  Ambamo ndege hutengeneza viota.+Naye korongo, miberoshi ndiyo nyumba yake.+ 18  Milima mirefu+ ni ya mbuzi wa milimani;+Miamba ni kimbilio la wibari.+ 19  Ameufanya mwezi kwa ajili ya nyakati zilizowekwa;+Jua linajua vema mahali linapotua.+ 20  Unasababisha giza, ili kuwe usiku;+Katika hilo wanyama wote wa porini hutembea. 21  Wana-simba wenye manyoya shingoni wananguruma kwa ajili ya mawindo+Na kwa ajili ya kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu mwenyewe.+ 22  Jua huanza kuangaza+​—⁠nao huondokaNao hujilaza katika mahali pao pa kujificha. 23  Mwanadamu huuendea utendaji wake+Na utumishi wake mpaka jioni.+ 24  Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova!+Zote umezifanya kwa hekima.+Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.+ 25  Na kwa habari ya bahari hii iliyo kubwa na pana,+Humo mna vitu vyenye kutambaa visivyo na hesabu,+Viumbe hai, vidogo kwa vikubwa.+ 26  Humo meli husafiri;+Naye Lewiathani,*+ yeye umemfanyiza ili achezecheze humo.+ 27  Wote hao—wanaendelea kukungojea wewe+Ili uwape chakula chao wakati wa majira yake.+ 28  Wao huokota kile unachowapa.+Unaufungua mkono wako—wanashiba vitu vyema.+ 29  Ukiuficha uso wako, wanaingiwa na wasiwasi.+Ukiiondoa roho yao, wanakata pumzi,+Na kurudi katika mavumbi yao.+ 30  Ukiituma roho yako, wanaumbwa;+Nawe unaufanya upya uso wa nchi. 31  Utukufu wa Yehova utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.+Yehova atashangilia kwa kazi zake.+ 32  Anaitazama dunia, nayo inatetemeka;+Anaigusa milima, nayo inatoa moshi.+ 33  Nitamwimbia Yehova katika maisha yangu yote;+Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+ 34  Kutafakari kwangu juu yake na kuwe kwenye kupendeza.+Mimi nami nitashangilia katika Yehova.+ 35  Watenda-dhambi watamalizwa kabisa kutoka duniani;+Nao waovu, hawatakuwapo tena.+Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu. Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini

Pengine mamba.