Zaburi 104:1-35
104 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu.+Ee Yehova Mungu wangu, umekuwa mkuu sana.+Umevaa utukufu na fahari,+
2 Unayejifunika nuru kama vazi,+Unayezitandaza mbingu kama hema,+
3 Yule anayejenga vyumba vyake vya juu kwa boriti katika maji,+Anayefanya mawingu kuwa gari lake,+Anayetembea juu ya mabawa ya upepo,+
4 Anayewafanya malaika zake kuwa roho,+Na wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza.+
5 Ameiwekea dunia msingi juu ya mahali pake palipofanywa imara;+Haitatikiswa mpaka wakati usio na kipimo, au milele.+
6 Uliifunika kwa kilindi cha maji kama kwa vazi.+Maji yalikuwa yamesimama juu ya milima.+
7 Yakaanza kukimbia ulipoyakemea;+Yakakimbia kwa wasiwasi mkubwa yaliposikia sauti ya mngurumo wako—
8 Milima ikapanda juu,+Nchi tambarare za mabonde zikashuka chini—Mpaka mahali ulipoyawekea msingi wake.
9 Uliweka mpaka, yasiupite,+Ili yasiifunike dunia tena.+
10 Anatuma mabubujiko ndani ya mabonde yenye vijito;+Yanaendelea kusonga mbele katikati ya milima.
11 Daima yanawapa maji ya kunywa wanyama wote wa porini;+Punda-milia+ hukata kiu yao kwa ukawaida.
12 Juu yake hukaa viumbe vinavyoruka vya mbinguni;+Kutoka katikati ya majani mengi yanaendelea kuvuma.+
13 Anainywesha maji milima kutoka katika vyumba vyake vya juu.+Dunia imeshiba matunda ya kazi zako.+
14 Anafanya majani mabichi yachipuke kwa ajili ya wanyama,+Na mimea ili itumikie wanadamu,+Ili chakula kitokezwe duniani,+
15 Na divai ambayo hufanya moyo wa mwanadamu anayeweza kufa ushangilie,+Kuufanya uso ung’ae kwa mafuta,+Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+
16 Miti ya Yehova imeshiba,Mierezi ya Lebanoni ambayo aliipanda.+
17 Ambamo ndege hutengeneza viota.+Naye korongo, miberoshi ndiyo nyumba yake.+
18 Milima mirefu+ ni ya mbuzi wa milimani;+Miamba ni kimbilio la wibari.+
19 Ameufanya mwezi kwa ajili ya nyakati zilizowekwa;+Jua linajua vema mahali linapotua.+
20 Unasababisha giza, ili kuwe usiku;+Katika hilo wanyama wote wa porini hutembea.
21 Wana-simba wenye manyoya shingoni wananguruma kwa ajili ya mawindo+Na kwa ajili ya kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu mwenyewe.+
22 Jua huanza kuangaza+—nao huondokaNao hujilaza katika mahali pao pa kujificha.
23 Mwanadamu huuendea utendaji wake+Na utumishi wake mpaka jioni.+
24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova!+Zote umezifanya kwa hekima.+Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.+
25 Na kwa habari ya bahari hii iliyo kubwa na pana,+Humo mna vitu vyenye kutambaa visivyo na hesabu,+Viumbe hai, vidogo kwa vikubwa.+
26 Humo meli husafiri;+Naye Lewiathani,*+ yeye umemfanyiza ili achezecheze humo.+
27 Wote hao—wanaendelea kukungojea wewe+Ili uwape chakula chao wakati wa majira yake.+
28 Wao huokota kile unachowapa.+Unaufungua mkono wako—wanashiba vitu vyema.+
29 Ukiuficha uso wako, wanaingiwa na wasiwasi.+Ukiiondoa roho yao, wanakata pumzi,+Na kurudi katika mavumbi yao.+
30 Ukiituma roho yako, wanaumbwa;+Nawe unaufanya upya uso wa nchi.
31 Utukufu wa Yehova utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.+Yehova atashangilia kwa kazi zake.+
32 Anaitazama dunia, nayo inatetemeka;+Anaigusa milima, nayo inatoa moshi.+
33 Nitamwimbia Yehova katika maisha yangu yote;+Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+
34 Kutafakari kwangu juu yake na kuwe kwenye kupendeza.+Mimi nami nitashangilia katika Yehova.+
35 Watenda-dhambi watamalizwa kabisa kutoka duniani;+Nao waovu, hawatakuwapo tena.+Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu. Msifuni Yah!+
Maelezo ya Chini
^ Pengine mamba.