Zaburi 33:1-22
33 Pigeni vigelegele vya shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+Sifa ni jambo linalofaa kwa wanyoofu.+
2 Mtoleeni Yehova shukrani kwa kinubi;+Mpigieni muziki kwa kinanda+ chenye nyuzi kumi.
3 Mwimbieni wimbo mpya;+Fanyeni yote mnayoweza katika kumpigia vinanda pamoja na vigelegele vya shangwe.+
4 Kwa maana neno la Yehova ni la unyoofu,+Nayo kazi yake yote ni kwa uaminifu.+
5 Anapenda uadilifu na haki.+Dunia imejawa na fadhili zenye upendo za Yehova.+
6 Mbingu zilifanywa kwa neno la Yehova,+Nayo majeshi yake yote yalifanywa kwa roho ya kinywa chake.+
7 Anayakusanya maji ya bahari kana kwamba ni kwa bwawa,+Akiweka katika maghala maji yenye kututumuka.
8 Wale wote walio wa dunia na wamwogope Yehova.+Wote wanaokaa katika nchi yenye kuzaa na wamhofu.+
9 Kwa maana yeye mwenyewe alisema, na ikawa hivyo;+Yeye mwenyewe alitoa amri, nayo ikasimama hivyo.+
10 Yehova mwenyewe amevunja shauri la mataifa;+Amezuia fikira za vikundi vya watu.+
11 Shauri la Yehova litasimama milele;+Mawazo ya moyo wake ni kwa kizazi kimoja baada ya kizazi kingine.+
12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+Watu ambao amewachagua wawe urithi wake.+
13 Kutoka mbinguni Yehova ametazama,+Amewaona wana wote wa binadamu.+
14 Kutoka katika mahali palipofanywa imara ambako yeye hukaa+Amewakazia macho wale wote wanaokaa duniani.
15 Anaifanyiza mioyo yao wote pamoja;+Anazifikiria kazi zao zote.+
16 Hakuna mfalme anayeokolewa kwa wingi wa majeshi yake;+Mtu mwenye nguvu haokolewi kwa wingi wa nguvu.+
17 Farasi ni udanganyifu kwa ajili ya wokovu,+Na kwa wingi wa nguvu zake haokoi.+
18 Tazama! Jicho la Yehova linawaelekea wale wanaomwogopa,+Wale wanaozingojea fadhili zake zenye upendo,+
19 Ili kuikomboa nafsi yao na kifo,+Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa.+
20 Nafsi yetu imekuwa ikimtarajia Yehova.+Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Kwa maana moyo wetu hushangilia katika yeye;+Kwa maana tumelitegemea jina lake takatifu.+
22 Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, na ziwe juu yetu,+Kwa vile tumeendelea kukungojea.+