Zaburi 110:1-7

Ya Daudi. Muziki. 110  Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni:+“Keti kwenye mkono wangu wa kuume+Mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.”+  Yehova ataituma fimbo+ ya nguvu zako kutoka Sayuni,+ akisema:“Nenda ukitiisha katikati ya adui zako.”+   Watu wako+ watajitoa kwa hiari+ katika siku ya jeshi lako.+Katika fahari za utakatifu,+ kutoka tumbo la uzazi la mapambazuko,Una kundi lako la vijana kama matone yaumande.+   Yehova ameapa+ (naye hatajuta):+“Wewe ni kuhani mpaka wakati usio na kipimo+Kwa mfano wa Melkizedeki!”+   Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume+Hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.+   Atatekeleza hukumu katikati ya mataifa;+Atafanya maiti zijae.+Hakika atamvunja vipande-vipande aliye kichwa juu ya nchi yenye hesabu kubwa ya watu.+   Kutoka katika bonde la mto njiani atakunywa.+Ndiyo sababu atakiinua kichwa chake juu.+

Maelezo ya Chini