Zaburi 40:1-17

Kwa kiongozi. Ya Daudi, muziki. 40  Nilimtumainia Yehova kwa bidii,+Kwa hiyo akanitegea sikio lake na kusikia kilio changu cha kuomba msaada.+   Yeye pia akaniinua kutoka katika shimo lenye kunguruma,+Kutoka katika matope ya nchi.+Kisha yeye akainua miguu yangu juu ya mwamba;+Akazifanya imara hatua zangu.+   Tena, akatia wimbo mpya katika kinywa changu,Sifa kwa Mungu wetu.+Wengi wataona hilo na kuogopa,+Nao watamtegemea Yehova.+   Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amemfanya Yehova kuwa tegemeo lake+Na ambaye hakuelekeza uso wake kwa watu wakaidi,Wala kwa wale wanaogeukia uwongo.+   Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+Hakuna wa kulinganishwa nawe.+Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+   Hukupendezwa na dhabihu na toleo;+Haya masikio yangu uliyafungua.+Hukutaka toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi.+   Kwa hiyo, nilisema: “Tazama nimekuja,+Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu.+   Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako,+Na sheria yako imo ndani yangu.+   Nimetangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+Tazama! Siizuii midomo yangu.+Ee Yehova, wewe mwenyewe unajua hivyo vema.+ 10  Uadilifu wako sikuufunika moyoni mwangu.+Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.+Sikuficha fadhili zako zenye upendo na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+ 11  Wewe mwenyewe, Ee Yehova, usinizuilie huruma zako.+Fadhili zako zenye upendo na ukweli wako zinilinde daima.+ 12  Kwa maana misiba ilinizunguka mpaka ikawa haihesabiki.+Makosa yangu mengi zaidi yalinifikia kuliko vile nilivyoweza kuona;+Yakawa mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,+Nao moyo wangu mwenyewe uliniacha.+ 13  Ee Yehova, upendezwe na kunikomboa.+Ee Yehova, ufanye haraka kuja kunisaidia.+ 14  Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+Wale wanaoitafuta nafsi yangu wapate kuifagilia mbali.+Wale wanaopendezwa na msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+ 15  Na wakodoe macho kwa mshangao kwa sababu ya aibu yao+Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”+ 16  Na hao washangilie na kukufurahia wewe,+Wale wote wanaokutafuta.+Na waseme daima: “Yehova na atukuzwe,”+Wale wanaopenda wokovu wako.+ 17  Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+Yehova mwenyewe ananijali.+Wewe ni msaidizi wangu na Mwokoaji wangu.+Ee Mungu wangu, usichelewe mno.+

Maelezo ya Chini