Zaburi 40:1-17
Kwa kiongozi. Ya Daudi, muziki.
40 Nilimtumainia Yehova kwa bidii,+Kwa hiyo akanitegea sikio lake na kusikia kilio changu cha kuomba msaada.+
2 Yeye pia akaniinua kutoka katika shimo lenye kunguruma,+Kutoka katika matope ya nchi.+Kisha yeye akainua miguu yangu juu ya mwamba;+Akazifanya imara hatua zangu.+
3 Tena, akatia wimbo mpya katika kinywa changu,Sifa kwa Mungu wetu.+Wengi wataona hilo na kuogopa,+Nao watamtegemea Yehova.+
4 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amemfanya Yehova kuwa tegemeo lake+Na ambaye hakuelekeza uso wake kwa watu wakaidi,Wala kwa wale wanaogeukia uwongo.+
5 Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+Hakuna wa kulinganishwa nawe.+Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+
6 Hukupendezwa na dhabihu na toleo;+Haya masikio yangu uliyafungua.+Hukutaka toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi.+
7 Kwa hiyo, nilisema: “Tazama nimekuja,+Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu.+
8 Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako,+Na sheria yako imo ndani yangu.+
9 Nimetangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+Tazama! Siizuii midomo yangu.+Ee Yehova, wewe mwenyewe unajua hivyo vema.+
10 Uadilifu wako sikuufunika moyoni mwangu.+Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.+Sikuficha fadhili zako zenye upendo na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+
11 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, usinizuilie huruma zako.+Fadhili zako zenye upendo na ukweli wako zinilinde daima.+
12 Kwa maana misiba ilinizunguka mpaka ikawa haihesabiki.+Makosa yangu mengi zaidi yalinifikia kuliko vile nilivyoweza kuona;+Yakawa mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,+Nao moyo wangu mwenyewe uliniacha.+
13 Ee Yehova, upendezwe na kunikomboa.+Ee Yehova, ufanye haraka kuja kunisaidia.+
14 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+Wale wanaoitafuta nafsi yangu wapate kuifagilia mbali.+Wale wanaopendezwa na msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+
15 Na wakodoe macho kwa mshangao kwa sababu ya aibu yao+Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”+
16 Na hao washangilie na kukufurahia wewe,+Wale wote wanaokutafuta.+Na waseme daima: “Yehova na atukuzwe,”+Wale wanaopenda wokovu wako.+
17 Lakini mimi ninateseka nami ni maskini.+Yehova mwenyewe ananijali.+Wewe ni msaidizi wangu na Mwokoaji wangu.+Ee Mungu wangu, usichelewe mno.+