Zaburi 17:1-15
Sala ya Daudi.
17 Usikie jambo la uadilifu, Ee Yehova; Usikilize kwa makini kilio changu cha kusihi;+Tega sikio kwa sala yangu bila midomo ya udanganyifu.+
2 Hukumu yangu na itoke mbele zako;+Macho yako mwenyewe na yaone unyoofu.+
3 Umeuchunguza moyo wangu, umefanya ukaguzi wakati wa usiku,+Umenisafisha; utagundua kwamba sijapanga hila.+Kinywa changu hakitafanya kosa.+
4 Nao utendaji wa wanadamu,Kwa maneno ya midomo yako mimi mwenyewe nimejilinda na njia za mnyang’anyi.+
5 Hatua zangu na zishike njia zako,+Ambamo hatua za miguu yangu hakika hazitatikiswa.+
6 Mimi mwenyewe nakuitia wewe, kwa sababu utanijibu, Ee Mungu.+Tega sikio lako kwangu. Usikilize neno langu.+
7 Uyafanye matendo yako ya fadhili zenye upendo yawe ya ajabu,+ Ee Mwokozi wa wale wanaotafuta kimbilioKutoka kwa waasi walio dhidi ya mkono wako wa kuume.+
8 Unitunze kama mboni ya jicho,+Katika kivuli cha mabawa yako unifiche,+
9 Kwa sababu ya waovu ambao wamenipora.Adui za nafsi yangu wanazidi kunizingira.+
10 Wamejizungushia mafuta yao wenyewe;+Kwa vinywa vyao wamesema kwa majivuno;+
11 Sasa wametuzingira hatua zetu;+Wanakaza macho yao ili kuelekeza duniani.+
12 Mfano wake ni ule wa simba anayetamani kurarua vipande-vipande+Na ule wa mwana-simba anayekaa mahali palipofichika.
13 Usimame, Ee Yehova; umkabili usoni;+Mfanye ainame; kwa upanga wako uiokoe nafsi yangu kutoka kwa mwovu,+
14 Kwa mkono wako, Ee Yehova, kutoka kwa watu,+Kutoka kwa watu wa mfumo huu wa mambo,+ ambao fungu lao liko katika maisha haya,+Na ambao tumbo lao wewe hulijaza kwa hazina iliyofichwa,+Ambao wametosheka na wana+Na ambao huwarundikia watoto wao vitu wanavyoacha.+
15 Nami, katika uadilifu nitauona uso wako;+Nitatosheka kuliona umbo lako ninapoamka.+