Zaburi 146:1-10

146  Msifuni Yah!+Msifu Yehova, Ee nafsi yangu.+   Nitamsifu Yehova muda wote wa maisha yangu.+Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+   Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo,+Wala katika mtu wa udongo, ambaye hana wokovu wowote.+   Roho yake hutoka,+ naye hurudi kwenye udongo wake;+Siku hiyo mawazo yake hupotea.+   Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,+Ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake,+   Mtengenezaji wa mbingu na dunia,+Wa bahari, na vyote vilivyomo,+Yeye anayedumisha ukweli mpaka wakati usio na kipimo,+   Yeye anayetekeleza hukumu kwa ajili ya waliopunjwa,+Yeye anayewapa wenye njaa mkate.+Yehova anawafungua wale waliofungwa.+   Yehova anafungua macho ya vipofu;+Yehova anawainua wale walioinama chini;+Yehova anawapenda waadilifu.+   Yehova anawalinda wakaaji wageni;+Humtuliza mvulana asiye na baba na mjane,+Lakini njia+ ya waovu yeye huipotosha.+ 10  Yehova atakuwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo,+Mungu wako, Ee Sayuni, kwa kizazi baada ya kizazi.+Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini