Zaburi 146:1-10
146 Msifuni Yah!+Msifu Yehova, Ee nafsi yangu.+
2 Nitamsifu Yehova muda wote wa maisha yangu.+Nitampigia Mungu wangu muziki maadamu nipo.+
3 Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo,+Wala katika mtu wa udongo, ambaye hana wokovu wowote.+
4 Roho yake hutoka,+ naye hurudi kwenye udongo wake;+Siku hiyo mawazo yake hupotea.+
5 Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,+Ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake,+
6 Mtengenezaji wa mbingu na dunia,+Wa bahari, na vyote vilivyomo,+Yeye anayedumisha ukweli mpaka wakati usio na kipimo,+
7 Yeye anayetekeleza hukumu kwa ajili ya waliopunjwa,+Yeye anayewapa wenye njaa mkate.+Yehova anawafungua wale waliofungwa.+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+Yehova anawainua wale walioinama chini;+Yehova anawapenda waadilifu.+
9 Yehova anawalinda wakaaji wageni;+Humtuliza mvulana asiye na baba na mjane,+Lakini njia+ ya waovu yeye huipotosha.+
10 Yehova atakuwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo,+Mungu wako, Ee Sayuni, kwa kizazi baada ya kizazi.+Msifuni Yah!+