Zaburi 50:1-23

Muziki wa Asafu.+ 50  Mwenye Uwezo,+ Mungu, Yehova,+ amesema mwenyewe,+Naye anaiita dunia,+Kutoka mashariki mpaka magharibi.+   Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu mwenyewe ameangaza.+   Mungu wetu atakuja naye hawezi kukaa kimya.+Mbele zake kuna moto unaoteketeza,+Na kumzunguka pande zote hali ya hewa imekuwa yenye dhoruba kali sana.+   Yeye anaziita mbingu juu na dunia+Ili atekeleze hukumu juu ya watu wake:+   “Wakusanye kwangu washikamanifu wangu,+Wale wanaofanya agano langu juu ya dhabihu.”+   Na mbingu zinasema juu ya uadilifu wake,+Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ Sela.   “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitasema,+Ee Israeli, nami nitatoa ushahidi dhidi yako.+Mimi ni Mungu, Mungu wako.+   Mimi siwakaripii kuhusiana na dhabihu zenu,+Wala kuhusiana na matoleo yako mazima ya kuteketezwa yaliyo mbele zangu daima.+   Sitachukua ng’ombe-dume katika nyumba yako,+Wala mbuzi-dume katika mazizi yako. 10  Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+Wanyama walio juu ya milima elfu moja.+ 11  Najua vizuri kila kiumbe chenye mabawa cha milimani,+Na makundi ya wanyama wa porini yako pamoja nami.+ 12  Ningalikuwa na njaa, singalikuambia;Kwa maana nchi yenye kuzaa+ na vyote vinavyoijaza ni vyangu.+ 13  Je, nile nyama ya ng’ombe-dume wenye nguvu,+Na je, ninywe damu ya mbuzi-dume?+ 14  Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+Na umtimizie Aliye Juu Zaidi nadhiri zako;+ 15  Na uniite katika siku ya taabu.+Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+ 16  Lakini Mungu atamwambia mwovu:+“Una haki gani ya kuyataja masharti yangu,+Na kwamba ulichukue agano langu kinywani mwako?+ 17  Tazama, wewe—wewe umechukia nidhamu,+Nawe unaendelea kuyatupa maneno yangu nyuma yako.+ 18  Wakati wowote ulipomwona mwizi, naam, ulipendezwa naye;+Nawe ulishirikiana na wazinzi.+ 19  Umefungua kinywa chako kutoa lililo baya,+Na ulimi wako unaushikamanisha na udanganyifu.+ 20  Unaketi na kusema vibaya juu ya ndugu yako mwenyewe,+Juu ya mwana wa mama yako unafichua kosa.+ 21  Umeyafanya mambo hayo, nami nikaendelea kukaa kimya.+Ulidhani kwamba kwa hakika mimi ningekuwa kama wewe.+Nitakukaripia,+ nami nitayarekebisha mambo mbele ya macho yako.+ 22  Tafadhali, enyi mnaomsahau Mungu eleweni hili,+Nisije nikawararua vipande-vipande bila ya kuwa na mkombozi.+ 23  Yule anayetoa shukrani zikiwa dhabihu yake ndiye anayenitukuza;+Naye anayedumisha njia iliyowekwa,Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+

Maelezo ya Chini