Zaburi 75:1-10
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.
75 Tunakutolea shukrani, Ee Mungu; tunakutolea shukrani,+Nalo jina lako liko karibu.+Lazima watu wazitangaze kazi zako za ajabu.+
2 “Kwa maana niliuchukua wakati uliowekwa;+Mimi nikaanza kuhukumu kwa unyoofu.+
3 Dunia na wakaaji wake wote wakiyeyuka,+Ni mimi niliyezirekebisha nguzo zake.”+ Sela.
4 Niliwaambia wapumbavu: “Msiwe wapumbavu,”+Na waovu: “Msiinue pembe.+
5 Msiinue pembe yenu juu.Msiseme mkiwa na shingo yenye kiburi.+
6 Kwa maana wala kutoka mashariki wala kutoka magharibi,Wala kutoka kusini hakutoki kuinuliwa.
7 Kwa maana Mungu ndiye mwamuzi.+Humshusha huyu, na kumwinua yule.+
8 Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova,+Kimejaa mchanganyiko, nayo divai inatoa povu.Na hakika kutoka hicho yeye atayamwaga machicha yake;Waovu wote wa dunia watayakamua, na kunywa.”+
9 Lakini mimi, nitaeleza juu ya hayo mpaka wakati usio na kipimo;Nitampigia muziki Mungu wa Yakobo.+
10 “Na pembe zote za waovu nitazikata.”+Pembe za mwadilifu zitainuliwa.+