Zaburi 75:1-10

Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo. 75  Tunakutolea shukrani, Ee Mungu; tunakutolea shukrani,+Nalo jina lako liko karibu.+Lazima watu wazitangaze kazi zako za ajabu.+   “Kwa maana niliuchukua wakati uliowekwa;+Mimi nikaanza kuhukumu kwa unyoofu.+   Dunia na wakaaji wake wote wakiyeyuka,+Ni mimi niliyezirekebisha nguzo zake.”+ Sela.   Niliwaambia wapumbavu: “Msiwe wapumbavu,”+Na waovu: “Msiinue pembe.+   Msiinue pembe yenu juu.Msiseme mkiwa na shingo yenye kiburi.+   Kwa maana wala kutoka mashariki wala kutoka magharibi,Wala kutoka kusini hakutoki kuinuliwa.   Kwa maana Mungu ndiye mwamuzi.+Humshusha huyu, na kumwinua yule.+   Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova,+Kimejaa mchanganyiko, nayo divai inatoa povu.Na hakika kutoka hicho yeye atayamwaga machicha yake;Waovu wote wa dunia watayakamua, na kunywa.”+   Lakini mimi, nitaeleza juu ya hayo mpaka wakati usio na kipimo;Nitampigia muziki Mungu wa Yakobo.+ 10  “Na pembe zote za waovu nitazikata.”+Pembe za mwadilifu zitainuliwa.+

Maelezo ya Chini