Zaburi 12:1-8
Kwa kiongozi katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.
12 Uniokoe,+ Ee Yehova, kwa maana mshikamanifu amefikia mwisho;+Kwa maana watu waaminifu wametoweka kutoka katikati ya wana wa binadamu.
2 Wao huendelea kusemezana mambo yasiyo ya kweli;+Kwa midomo laini+ wao huendelea kusema wakiwa na mioyo miwili.+
3 Yehova ataikata midomo yote iliyo laini,Ulimi unaosema maneno makuu,+
4 Wale ambao wamesema: “Kwa ulimi wetu tutashinda.+Midomo yetu iko pamoja nasi. Ni nani atakayekuwa bwana kwetu?”
5 “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+“Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+
6 Maneno ya Yehova ni maneno safi,+Kama fedha iliyosafishwa katika tanuru ya kuyeyushia kwenye udongo, iliyosafishwa mara saba.
7 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, utawalinda;+Utamhifadhi kila mmoja kutokana na kizazi hiki mpaka wakati usio na kipimo.
8 Waovu wanatembea kuzunguka pande zote,Kwa sababu uovu unatukuzwa katikati ya wana wa binadamu.+