Zaburi 12:1-8

Kwa kiongozi katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi. 12  Uniokoe,+ Ee Yehova, kwa maana mshikamanifu amefikia mwisho;+Kwa maana watu waaminifu wametoweka kutoka katikati ya wana wa binadamu.   Wao huendelea kusemezana mambo yasiyo ya kweli;+Kwa midomo laini+ wao huendelea kusema wakiwa na mioyo miwili.+   Yehova ataikata midomo yote iliyo laini,Ulimi unaosema maneno makuu,+   Wale ambao wamesema: “Kwa ulimi wetu tutashinda.+Midomo yetu iko pamoja nasi. Ni nani atakayekuwa bwana kwetu?”   “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+“Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+   Maneno ya Yehova ni maneno safi,+Kama fedha iliyosafishwa katika tanuru ya kuyeyushia kwenye udongo, iliyosafishwa mara saba.   Wewe mwenyewe, Ee Yehova, utawalinda;+Utamhifadhi kila mmoja kutokana na kizazi hiki mpaka wakati usio na kipimo.   Waovu wanatembea kuzunguka pande zote,Kwa sababu uovu unatukuzwa katikati ya wana wa binadamu.+

Maelezo ya Chini