Zaburi 118:1-29

118  Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+   Israeli na aseme sasa:“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+   Wale wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:+“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+   Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:+“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+   Kutoka katika hali zenye kutaabisha nilimwitia Yah;+Yah akanijibu na kuniweka katika mahali penye nafasi pana.+   Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+Mtu wa udongo anaweza kunitenda nini?+   Yehova yuko upande wangu kati ya wale wanaonisaidia,+Hivi kwamba mimi nitawatazama wale wanaonichukia.+   Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+Kuliko kumtegemea mtu wa udongo.+   Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+Kuliko kuwategemea watu wenye vyeo.+ 10  Mataifa yote yalinizunguka.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+ 11  Walinizingira, naam, walikuwa wamenizingira.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova. 12  Walinizunguka kama nyuki;+Walizimwa kama moto wa vichaka vya miiba.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+ 13  Ulinisukuma kwa nguvu ili nianguke,+Lakini Yehova mwenyewe alinisaidia.+ 14  Yah ni kinga yangu na nguvu zangu,+Naye huwa wokovu kwangu.+ 15  Sauti ya vigelegele vya shangwe na wokovu+Imo katika mahema+ ya waadilifu.+Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+ 16  Mkono wa kuume wa Yehova unajiinua;+Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+ 17  Sitakufa, bali nitaendelea kuishi,+Ili nizitangaze kazi za Yah.+ 18  Yah alinirekebisha vikali,+Lakini hakunitia mikononi mwa kifo.+ 19  Nifungulieni malango ya uadilifu.+Mimi nitayaingia; nitamsifu Yah.+ 20  Hili ndilo lango la Yehova.+Waadilifu wataliingia.+ 21  Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+Nawe ukawa wokovu wangu.+ 22  Jiwe ambalo wajenzi walilikataa+Limekuwa jiwe kuu la pembeni.+ 23  Hili limetokana na Yehova mwenyewe;+Ni la ajabu machoni petu.+ 24  Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;+Tutaishangilia na kuifurahia.+ 25  Ah, sasa, Yehova, uokoe, tafadhali!+Ah, sasa, Yehova, ufanikishe, tafadhali!+ 26  Na abarikiwe Yeye anayekuja katika jina la Yehova;+Tumewabariki ninyi watu kutoka katika nyumba ya Yehova.+ 27  Yehova ndiye Mungu,+Naye hutupa nuru.+Fungeni maandamano ya sherehe+ kwa matawi,+Mpaka kwenye pembe za madhabahu.+ 28  Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;+Mungu wangu⁠—​nitakutukuza.+ 29  Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

Maelezo ya Chini