Zaburi 118:1-29
118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
2 Israeli na aseme sasa:“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
3 Wale wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:+“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:+“Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+
5 Kutoka katika hali zenye kutaabisha nilimwitia Yah;+Yah akanijibu na kuniweka katika mahali penye nafasi pana.+
6 Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+Mtu wa udongo anaweza kunitenda nini?+
7 Yehova yuko upande wangu kati ya wale wanaonisaidia,+Hivi kwamba mimi nitawatazama wale wanaonichukia.+
8 Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+Kuliko kumtegemea mtu wa udongo.+
9 Ni afadhali kupata kimbilio katika Yehova+Kuliko kuwategemea watu wenye vyeo.+
10 Mataifa yote yalinizunguka.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+
11 Walinizingira, naam, walikuwa wamenizingira.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.
12 Walinizunguka kama nyuki;+Walizimwa kama moto wa vichaka vya miiba.+Nami niliendelea kuwazuilia mbali katika jina la Yehova.+
13 Ulinisukuma kwa nguvu ili nianguke,+Lakini Yehova mwenyewe alinisaidia.+
14 Yah ni kinga yangu na nguvu zangu,+Naye huwa wokovu kwangu.+
15 Sauti ya vigelegele vya shangwe na wokovu+Imo katika mahema+ ya waadilifu.+Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+
16 Mkono wa kuume wa Yehova unajiinua;+Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu.+
17 Sitakufa, bali nitaendelea kuishi,+Ili nizitangaze kazi za Yah.+
18 Yah alinirekebisha vikali,+Lakini hakunitia mikononi mwa kifo.+
19 Nifungulieni malango ya uadilifu.+Mimi nitayaingia; nitamsifu Yah.+
20 Hili ndilo lango la Yehova.+Waadilifu wataliingia.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+Nawe ukawa wokovu wangu.+
22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa+Limekuwa jiwe kuu la pembeni.+
23 Hili limetokana na Yehova mwenyewe;+Ni la ajabu machoni petu.+
24 Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;+Tutaishangilia na kuifurahia.+
25 Ah, sasa, Yehova, uokoe, tafadhali!+Ah, sasa, Yehova, ufanikishe, tafadhali!+
26 Na abarikiwe Yeye anayekuja katika jina la Yehova;+Tumewabariki ninyi watu kutoka katika nyumba ya Yehova.+
27 Yehova ndiye Mungu,+Naye hutupa nuru.+Fungeni maandamano ya sherehe+ kwa matawi,+Mpaka kwenye pembe za madhabahu.+
28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;+Mungu wangu—nitakutukuza.+
29 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+