Zaburi 45:1-17
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi. Ya wana wa Kora. Maskili. Wimbo wa wanawake wapendwa.
45 Moyo wangu umesisimuka kwa sababu ya jambo jema.+Ninasema: “Kazi zangu zinamhusu mfalme.”+Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mwandikaji stadi.+
2 Kwa kweli wewe una sura nzuri kuliko wana wa binadamu.+Uvutio umemiminwa juu ya midomo yako.+Ndiyo sababu Mungu amekubariki mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Funga upanga+ wako kwenye paja lako, ewe mwenye nguvu,+Pamoja na utukufu wako na fahari yako.+
4 Na katika fahari yako endelea mpaka ufanikiwe;+Panda kwa kutetea kweli na unyenyekevu na uadilifu,+Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo yenye kuogopesha.+
5 Mishale yako ni mikali—vikundi vya watu vinaendelea kuanguka chini yako+—Katika moyo wa adui za mfalme.+
6 Mungu ni kiti chako cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele;+Fimbo ya enzi ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.+
7 Umependa uadilifu+ nawe unachukia uovu.+Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako,+ amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.+
8 Mavazi yako yote ni manemane na udi na kida;+Kutoka katika jumba kuu la mfalme la pembe,+ vinanda vimekufanya ushangilie.
9 Binti+ za wafalme wamo kati ya wanawake wako wenye thamani.Malkia+ amesimama kwenye mkono wako wa kuume akiwa amevaa dhahabu ya Ofiri.+
10 Sikiliza, ewe binti, uone, na utege sikio lako;Na uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.+
11 Naye mfalme atautamani urembo wako,+Kwa maana yeye ni bwana wako,+Kwa hiyo mwinamie.+
12 Binti Tiro na zawadi pia+—Walio matajiri kati ya watu watautuliza uso wako mwenyewe.+
13 Binti ya mfalme ana utukufu wote ndani ya nyumba;+Mavazi yake yamepambwa kwa dhahabu.
14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa.+Mabikira katika msafara wake ambao ni rafiki zake wanaingizwa ndani kwako.+
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe;Wataingia katika jumba la mfalme.
16 Mahali pa mababu+ zako patachukuliwa na wana wako,+Ambao utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+
17 Nitalitaja jina lako katika vizazi vyote vitakavyokuja.+Ndiyo sababu vikundi vya watu vitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.