Zaburi 81:1-16

Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya Asafu. 81  Mpigieni Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe;+Mpigieni Mungu wa Yakobo kelele za ushindi.+   Anzisheni muziki+ na kuchukua tari,+Kinubi chenye kupendeza pamoja na kinanda.+   Katika mwezi mpya, pigeni baragumu;+Katika mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+   Kwa maana ni sharti kwa ajili ya Israeli,+Uamuzi wa hukumu wa Mungu wa Yakobo.   Alimwamuru Yosefu liwe kikumbusho,+Alipokuwa akipita juu ya nchi ya Misri.+Lugha ambayo sikuijua, niliendelea kuisikia.+   “Nililigeuza bega lake liondoke kwenye mzigo;+Mikono yake ikaondoka kwenye kikapu.+   Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+Nikaanza kukujibu katika mahali palipofichika pa mngurumo.+Nikakuchunguza kando ya maji ya Meriba.+ Sela.   Sikieni, enyi watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu,+Ee Israeli, ikiwa utanisikiliza.+   Katikati yako hakutakuwa na mungu yeyote mgeni;+Wala hutamwinamia mungu wa kigeni.+ 10  Mimi, Yehova, ni Mungu wako,+Yule anayekutoa katika nchi ya Misri.+Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+ 11  Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;+Na Israeli hakuonyesha utayari wowote kunielekea.+ 12  Na kwa hiyo nikawaacha waende katika ukaidi wa moyo wao;+Wakatembea katika mashauri yao wenyewe.+ 13  Laiti watu wangu wangekuwa wakinisikiliza,+Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+ 14  Adui zao ningewatiisha kwa urahisi,+Nami ningegeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+ 15  Na wale wanaomchukia Yehova vikali, watakuja kwake wakitetemeka,+Na wakati wao utakuwa mpaka wakati usio na kipimo. 16  Naye ataendelea kumlisha mafuta ya ngano,+Na kutokana na mwamba nitakushibisha asali.”+

Maelezo ya Chini