Zaburi 81:1-16
Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya Asafu.
81 Mpigieni Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe;+Mpigieni Mungu wa Yakobo kelele za ushindi.+
2 Anzisheni muziki+ na kuchukua tari,+Kinubi chenye kupendeza pamoja na kinanda.+
3 Katika mwezi mpya, pigeni baragumu;+Katika mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+
4 Kwa maana ni sharti kwa ajili ya Israeli,+Uamuzi wa hukumu wa Mungu wa Yakobo.
5 Alimwamuru Yosefu liwe kikumbusho,+Alipokuwa akipita juu ya nchi ya Misri.+Lugha ambayo sikuijua, niliendelea kuisikia.+
6 “Nililigeuza bega lake liondoke kwenye mzigo;+Mikono yake ikaondoka kwenye kikapu.+
7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+Nikaanza kukujibu katika mahali palipofichika pa mngurumo.+Nikakuchunguza kando ya maji ya Meriba.+ Sela.
8 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu,+Ee Israeli, ikiwa utanisikiliza.+
9 Katikati yako hakutakuwa na mungu yeyote mgeni;+Wala hutamwinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,+Yule anayekutoa katika nchi ya Misri.+Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;+Na Israeli hakuonyesha utayari wowote kunielekea.+
12 Na kwa hiyo nikawaacha waende katika ukaidi wa moyo wao;+Wakatembea katika mashauri yao wenyewe.+
13 Laiti watu wangu wangekuwa wakinisikiliza,+Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+
14 Adui zao ningewatiisha kwa urahisi,+Nami ningegeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+
15 Na wale wanaomchukia Yehova vikali, watakuja kwake wakitetemeka,+Na wakati wao utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.
16 Naye ataendelea kumlisha mafuta ya ngano,+Na kutokana na mwamba nitakushibisha asali.”+