Zaburi 145:1-21

Sifa, ya Daudi. א [ʼAʹleph] 145  Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mfalme,+Nami nitalibariki jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+ ב [Behth]   Mchana kutwa nitakubariki,+Nami nitalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+ ג [Giʹmel]   Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana,+Na ukuu wake hauchunguziki.+ ד [Daʹleth]   Kizazi baada ya kizazi kitazipongeza kazi zako,+Nao watatangaza juu ya matendo yako ya nguvu.+ ה [Heʼ]   Fahari tukufu ya utukufu wako+Na mambo ya kazi zako za ajabu nitayafanya yawe hangaiko langu.+ ו [Waw]   Nao wataongea juu ya nguvu za mambo yako yenye kuogopesha;+Nami nitautangaza ukuu wako.+ ז [Zaʹyin]   Watabubujikwa na maneno wakitaja wingi wa wema wako,+Na kwa sababu ya uadilifu wako watapiga vigelegele vya shangwe.+ ח [Chehth]   Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema,+Si mwepesi wa hasira naye ni mkuu katika fadhili zenye upendo.+ ט [Tehth]   Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema zake ziko juu ya kazi zake zote.+ י [Yohdh] 10  Kazi zako zote zitakusifu, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+ כ [Kaph] 11  Wataongea juu ya utukufu wa ufalme wako,+Nao watasema juu ya nguvu zako,+ ל [Laʹmedh] 12  Kuwajulisha wana wa binadamu matendo yake yenye nguvu+Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.+ מ [Mem] 13  Ufalme wako ni ufalme kwa nyakati zote zisizo na kipimo,+Na mamlaka yako ni ya kuendelea mpaka vizazi vyote vinavyofuata.+ ס [Saʹmekh] 14  Yehova anawategemeza wote wanaoanguka,+naye anawainua wote ambao wameinama chini.+ ע [ʽAʹyin] 15  Macho ya wote yanakutazama yakiwa na tumaini,+Nawe unawapa chakula chao katika majirayake.+ פ [Peʼ] 16  Unaufumbua mkono wako+Na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+ צ [Tsa·dhehʹ] 17  Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+Na mshikamanifu katika kazi zake zote.+ ק [Qohph] 18  Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.+ ר [Rehsh] 19  Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,+Naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.+ ש [Shin] 20  Yehova anawalinda wale wote wanaompenda,+Lakini atawaangamiza waovu wote.+ ת [Taw] 21  Kinywa changu kitasema sifa za Yehova;+Na wote wenye mwili na walibariki jina lake takatifu mpaka wakati usio na kipimo, hata milele.+

Maelezo ya Chini