Zaburi 145:1-21
Sifa, ya Daudi.
א [ʼAʹleph]
145 Nitakutukuza, Ee Mungu wangu Mfalme,+Nami nitalibariki jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
ב [Behth]
2 Mchana kutwa nitakubariki,+Nami nitalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
ג [Giʹmel]
3 Yehova ni mkuu na wa kusifiwa sana,+Na ukuu wake hauchunguziki.+
ד [Daʹleth]
4 Kizazi baada ya kizazi kitazipongeza kazi zako,+Nao watatangaza juu ya matendo yako ya nguvu.+
ה [Heʼ]
5 Fahari tukufu ya utukufu wako+Na mambo ya kazi zako za ajabu nitayafanya yawe hangaiko langu.+
ו [Waw]
6 Nao wataongea juu ya nguvu za mambo yako yenye kuogopesha;+Nami nitautangaza ukuu wako.+
ז [Zaʹyin]
7 Watabubujikwa na maneno wakitaja wingi wa wema wako,+Na kwa sababu ya uadilifu wako watapiga vigelegele vya shangwe.+
ח [Chehth]
8 Yehova ni mwenye neema na mwenye rehema,+Si mwepesi wa hasira naye ni mkuu katika fadhili zenye upendo.+
ט [Tehth]
9 Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema zake ziko juu ya kazi zake zote.+
י [Yohdh]
10 Kazi zako zote zitakusifu, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+
כ [Kaph]
11 Wataongea juu ya utukufu wa ufalme wako,+Nao watasema juu ya nguvu zako,+
ל [Laʹmedh]
12 Kuwajulisha wana wa binadamu matendo yake yenye nguvu+Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.+
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme kwa nyakati zote zisizo na kipimo,+Na mamlaka yako ni ya kuendelea mpaka vizazi vyote vinavyofuata.+
ס [Saʹmekh]
14 Yehova anawategemeza wote wanaoanguka,+naye anawainua wote ambao wameinama chini.+
ע [ʽAʹyin]
15 Macho ya wote yanakutazama yakiwa na tumaini,+Nawe unawapa chakula chao katika majirayake.+
פ [Peʼ]
16 Unaufumbua mkono wako+Na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+
צ [Tsa·dhehʹ]
17 Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+Na mshikamanifu katika kazi zake zote.+
ק [Qohph]
18 Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.+
ר [Rehsh]
19 Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,+Naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.+
ש [Shin]
20 Yehova anawalinda wale wote wanaompenda,+Lakini atawaangamiza waovu wote.+
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitasema sifa za Yehova;+Na wote wenye mwili na walibariki jina lake takatifu mpaka wakati usio na kipimo, hata milele.+