Zaburi 41:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayetenda kwa kumfikiria mtu wa hali ya chini;+Katika siku ya msiba Yehova atamwokoa.+
2 Yehova mwenyewe atamlinda na kumhifadhi hai.+Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+Nawe huwezi kamwe kumtia mkononi mwa nafsi ya adui zake.+
3 Yehova mwenyewe atamtegemeza katika kitanda cha ugonjwa;+Kitanda chake chote hakika utakibadilisha wakati wa ugonjwa wake.+
4 Mimi nami, nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+Uiponye nafsi yangu, kwa maana nimekutendea dhambi.”+
5 Nao adui zangu, wanasema mabaya juu yangu:+“Atakufa wakati gani na jina lake kwa kweli lipotee?”
6 Na mtu akija kuniona, moyo wake utasema mambo yasiyo ya kweli;+Atajikusanyia jambo lenye kuumiza;
Atatoka nje; huko nje atalisema.+
7 Wote wanaonichukia wananong’onezana juu yangu kwa muungano;+Wanaendelea kupanga hila ya jambo baya juu yangu:+
8 “Jambo lisilofaa kitu linamiminwa juu yake;+Sasa kwa kuwa amelala chini, hatasimama tena.”+
9 Pia mtu mwenye kuwa na amani nami, ambaye nimemtegemea,+Ambaye alikuwa akila mkate wangu,+ amekiinua kisigino chake dhidi yangu.+
10 Wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali na kuniinua,+Ili nipate kuwalipa.+
11 Kwa jambo hili ninajua kwamba umependezwa nami,Kwa sababu adui yangu hapigi kelele za ushindi juu yangu.+
12 Nami, umenitegemeza kwa sababu ya utimilifu wangu,+Nawe utaniweka mbele za uso wako mpaka wakati usio na kipimo.+
13 Yehova Mungu wa Israeli na abarikiwe+Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.+Amina na Amina.+