Zaburi 90:1-17
Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+
90 Ee Yehova, wewe mwenyewe umekuwa makao yetu halisi+Kwa kizazi baada ya kizazi.+
2 Kabla ya kuzaliwa kwa milima,+Au kutokezwa kwa dunia+ na nchi yenye kuzaa kana kwamba kwa maumivu ya kuzaa,+Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo wewe ni Mungu.+
3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi kuwa kitu kilichopondwa,+Nawe unasema: “Rudini, enyi wana wa binadamu.”+
4 Kwa maana miaka elfu machoni pako ni kama jana ikiisha kupita,+Na kama kesha la usiku.+
5 Umewafagilia mbali;+ wanakuwa usingizi tu;+Asubuhi, wao ni kama majani mabichi ambayo hubadilika.+
6 Asubuhi huchanua maua na lazima yabadilike;+Jioni, hunyauka na hakika hukauka.+
7 Kwa maana tumefikia mwisho kwa hasira yako,+Na kwa ghadhabu yako tumetiwa wasiwasi.+
8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+
9 Kwa maana siku zetu zote zimepungua katika ghadhabu yako;+Tumeimaliza miaka yetu kama mnong’ono tu.+
10 Kwa maana siku za miaka yetu ni miaka 70;+Na ikiwa kwa sababu ya nguvu za pekee ni miaka 80,+Hata hivyo hizo husisitiza kuleta taabu na mambo yenye kuumiza;+Kwa maana lazima zipite upesi, nasi huruka na kwenda zetu.+
11 Ni nani anayejua nguvu za hasira yako+Na ghadhabu yako kulingana na kukuogopa wewe?+
12 Utuonyeshe jinsi ya kuzihesabu siku zetu hivi kwamba+Tupate kuuingiza moyo wa hekima.+
13 Urudi, Ee Yehova!+ Mpaka wakati gani?+Nawe ujute juu ya watumishi wako.+
14 Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako zenye upendo,+Ili tupate kupiga vigelegele kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.+
15 Utufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+Miaka ambayo tumeona msiba.+
16 Utendaji wako na uonekane kwa watumishi wako+Na fahari yako juu ya wana wao.+
17 Nao uzuri wa Yehova Mungu wetu na uwe juu yetu,+Na kazi ya mikono yetu uifanye imara juu yetu.+Naam, kazi ya mikono yetu, uifanye imara.+