Zaburi 80:1-19

Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki. 80  Ee Mchungaji wa Israeli, tega sikio,+Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi.+Wewe unayeketi juu ya makerubi,+ uangaze.+   Mbele ya Efraimu na Benyamini na Manase, uamshe nguvu zako,+Na uje kutuokoa.+   Ee Mungu, uturudishe;+Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+   Ee Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea kuwaka hasira juu ya sala ya watu wako mpaka wakati gani?+   Umewalisha mkate wa machozi,+Nawe unaendelea kuwafanya wanywe machozi kwa machozi kwa kiasi kikubwa.+   Ulituweka tugombane na jirani zetu,+Nao adui zetu wanaendelea kudharau kama wanavyopenda.+   Ee Mungu wa majeshi, uturudishe;+Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+   Ulifanya mzabibu uondoke Misri.+Ukaendelea kuyafukuza mataifa, ili uupande.+   Ulitengeneza nafasi mbele yake,+ ili upate kutia mizizi na kuijaza nchi.+ 10  Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.+ 11  Hatua kwa hatua uliyaeneza matawi yake mpaka baharini,+Na machipukizi yake mpaka kwenye ule Mto.+ 12  Kwa nini umebomoa kuta zake za mawe,+Na kwa nini wale wote wanaopita barabarani wameuchuma?+ 13  Nguruwe-mwitu kutoka msituni anaendelea kuula,+Na makundi ya wanyama wa porini wanaendelea kuula.+ 14  Ee Mungu wa majeshi, urudi, tafadhali;+Utazame chini kutoka mbinguni, uone na kuutunza mzabibu huu,+ 15  Na shina ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+Na umtazame mwana ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+ 16  Huo umeteketezwa kwa moto, umekatwa.+Wanaangamia kutokana na kemeo la uso wako.+ 17  Mkono wako na uwe juu yake mtu wa mkono wako wa kuume,+Juu ya mwana wa binadamu ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+ 18  Nasi hatutageuka kutoka kwako.+Utuhifadhi hai, ili tupate kuliitia jina lako.+ 19  Ee Yehova Mungu wa majeshi, uturudishe;+Uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+

Maelezo ya Chini