Zaburi 55:1-23
Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi.
55 Utege sikio, Ee Mungu, kwa sala yangu;+Wala usijifiche kutoka kwa ombi langu la kutaka kibali.+
2 Unisikilize kwa makini na kunijibu.+Mahangaiko yangu yananisukuma huku na huku bila kuwa na utulivu,+Sina jambo lingine la kufanya ila kuonyesha wasiwasi.
3 Kwa sababu ya sauti ya adui, kwa sababu ya mkazo wa yule mwovu.+Kwa maana wanaendelea kuniangushia mambo yenye kuumiza,+Na kwa hasira wanadumisha uadui juu yangu.+
4 Moyo wangu una maumivu makali ndani yangu,+Na woga wa kifo umeniangukia.+
5 Woga, naam, kutetemeka kunaingia ndani yangu,+Na mtetemeko unanifunika.
6 Nami naendelea kusema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa!+Ningeruka mbali na kukaa.+
7 Tazama! ningeruka mbali;+Ningekaa nyikani.+—Sela—
8 Ningefanya haraka kwenda mahali pangu pa kuponyokeaKutokana na upepo wenye kuvuma, kutokana na tufani.”+
9 Uwavuruge, Ee Yehova, ugawanye ulimi wao,+Kwa maana nimeona jeuri na kuzozana jijini.+
10 Mchana na usiku wanalizunguka pande zote juu ya kuta zake;+Na mambo yenye kuumiza na taabu ziko ndani yake.+
11 Shida ziko ndani yake;Na katika viwanja vyake vya watu wote ukandamizaji na udanganyifu haujaondoka.+
12 Kwa maana sikushutumiwa na adui;+Kama ndivyo ningaliweza kuvumilia hilo.Si mtu anayenichukia vikali aliyejivuna sana dhidi yangu;+Kama ndivyo ningaliweza kujificha kutoka kwake.+
13 Lakini ilikuwa ni wewe, mwanadamu anayeweza kufa tunayelingana,+Mtu tunayejuana na ambaye ni rafiki yangu,+
14 Kwa sababu tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki ulio mtamu;+Tulikuwa tukitembea kuingia katika nyumba ya Mungu pamoja na watu wengi.+
15 Ukiwa na uwe juu yao!+Na washuke katika Kaburi* wakiwa hai;+Kwa maana wakati wao wa kukaa ugenini mambo mabaya yamekuwa ndani yao.+
16 Mimi nami nitamlilia Mungu;+Na Yehova mwenyewe ataniokoa.+
17 Jioni na asubuhi na katikati ya mchana sikosi kuhangaika nami naomboleza,+Naye huisikia sauti yangu.+
18 Hakika ataikomboa na kuiweka nafsi yangu katika amani mbali na vita vinavyofanywa juu yangu,+Kwa maana wakiwa umati wamekuja kuwa dhidi yangu.+
19 Mungu atasikia na kuwajibu,+Naam, Yeye anayeketi juu ya kiti cha ufalme kama zamani+—Sela—Wale ambao hawafanyi mabadiliko+Na ambao hawajamwogopa Mungu.+
20 Amenyoosha mikono yake dhidi ya wale walio na amani pamoja naye;+Amelitia unajisi agano lake.+
21 Maneno ya kinywa chake ni laini kuliko siagi,+Lakini moyo wake una mwelekeo wa kupigana.+Maneno yake ni laini kuliko mafuta,+Lakini ni panga zilizochomolewa.+
22 Mtupie Yehova mzigo wako,+Naye mwenyewe atakutegemeza.+Hatamwacha kamwe mwadilifu atikisike.+
23 Lakini wewe mwenyewe, Ee Mungu, utawashusha mpaka kwenye shimo lililo chini kabisa.+Nao watu wenye hatia ya damu na wadanganyifu, hawataishi nusu ya siku zao.+Lakini mimi, nitakutegemea wewe.+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.