Zaburi 55:1-23

Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi. 55  Utege sikio, Ee Mungu, kwa sala yangu;+Wala usijifiche kutoka kwa ombi langu la kutaka kibali.+   Unisikilize kwa makini na kunijibu.+Mahangaiko yangu yananisukuma huku na huku bila kuwa na utulivu,+Sina jambo lingine la kufanya ila kuonyesha wasiwasi.   Kwa sababu ya sauti ya adui, kwa sababu ya mkazo wa yule mwovu.+Kwa maana wanaendelea kuniangushia mambo yenye kuumiza,+Na kwa hasira wanadumisha uadui juu yangu.+   Moyo wangu una maumivu makali ndani yangu,+Na woga wa kifo umeniangukia.+   Woga, naam, kutetemeka kunaingia ndani yangu,+Na mtetemeko unanifunika.   Nami naendelea kusema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa!+Ningeruka mbali na kukaa.+   Tazama! ningeruka mbali;+Ningekaa nyikani.+Sela   Ningefanya haraka kwenda mahali pangu pa kuponyokeaKutokana na upepo wenye kuvuma, kutokana na tufani.”+   Uwavuruge, Ee Yehova, ugawanye ulimi wao,+Kwa maana nimeona jeuri na kuzozana jijini.+ 10  Mchana na usiku wanalizunguka pande zote juu ya kuta zake;+Na mambo yenye kuumiza na taabu ziko ndani yake.+ 11  Shida ziko ndani yake;Na katika viwanja vyake vya watu wote ukandamizaji na udanganyifu haujaondoka.+ 12  Kwa maana sikushutumiwa na adui;+Kama ndivyo ningaliweza kuvumilia hilo.Si mtu anayenichukia vikali aliyejivuna sana dhidi yangu;+Kama ndivyo ningaliweza kujificha kutoka kwake.+ 13  Lakini ilikuwa ni wewe, mwanadamu anayeweza kufa tunayelingana,+Mtu tunayejuana na ambaye ni rafiki yangu,+ 14  Kwa sababu tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki ulio mtamu;+Tulikuwa tukitembea kuingia katika nyumba ya Mungu pamoja na watu wengi.+ 15  Ukiwa na uwe juu yao!+Na washuke katika Kaburi* wakiwa hai;+Kwa maana wakati wao wa kukaa ugenini mambo mabaya yamekuwa ndani yao.+ 16  Mimi nami nitamlilia Mungu;+Na Yehova mwenyewe ataniokoa.+ 17  Jioni na asubuhi na katikati ya mchana sikosi kuhangaika nami naomboleza,+Naye huisikia sauti yangu.+ 18  Hakika ataikomboa na kuiweka nafsi yangu katika amani mbali na vita vinavyofanywa juu yangu,+Kwa maana wakiwa umati wamekuja kuwa dhidi yangu.+ 19  Mungu atasikia na kuwajibu,+Naam, Yeye anayeketi juu ya kiti cha ufalme kama zamani+SelaWale ambao hawafanyi mabadiliko+Na ambao hawajamwogopa Mungu.+ 20  Amenyoosha mikono yake dhidi ya wale walio na amani pamoja naye;+Amelitia unajisi agano lake.+ 21  Maneno ya kinywa chake ni laini kuliko siagi,+Lakini moyo wake una mwelekeo wa kupigana.+Maneno yake ni laini kuliko mafuta,+Lakini ni panga zilizochomolewa.+ 22  Mtupie Yehova mzigo wako,+Naye mwenyewe atakutegemeza.+Hatamwacha kamwe mwadilifu atikisike.+ 23  Lakini wewe mwenyewe, Ee Mungu, utawashusha mpaka kwenye shimo lililo chini kabisa.+Nao watu wenye hatia ya damu na wadanganyifu, hawataishi nusu ya siku zao.+Lakini mimi, nitakutegemea wewe.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.