Zaburi 43:1-5
43 Unihukumu,+ Ee Mungu,
Na uendeshe kesi+ yangu dhidi ya taifa lisilo shikamanifu.Uniokoe kutoka kwa mtu wa udanganyifu na mwenye kukosa uadilifu.+
2 Kwa maana wewe ni Mungu wa ngome yangu.+Kwa nini umenitupilia mbali?Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?+
3 Tuma nuru yako na kweli yako.+Na hivyo vyenyewe viniongoze.+Navyo vinilete kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye maskani yako kuu.+
4 Nami nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+Kwa Mungu, ambaye ni kushangilia kwangu kwa furaha.+Nami nitakusifu kwa kinubi, Ee Mungu, Mungu wangu.+
5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+