Zaburi 93:1-5
93 Yehova mwenyewe amekuwa mfalme!+Amevaa adhama;+Yehova amevaa—amejifunga mshipi wa nguvu.+Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isipate kutikiswa.+
2 Kiti chako cha ufalme kimefanywa imara tangu zamani za kale;+Wewe ni wa tangu wakati usio na kipimo.+
3 Mito imepaaza, Ee Yehova,Mito imepaaza sauti yake;+Mito inaendelea kupaaza mivumo yake.+
4 Juu ya sauti ya maji mengi, mashuu makubwa ya bahari,+Yehova ni mwenye fahari+ katika kilele.
5 Vikumbusho vyako vimekuwa vyenye kutegemeka sana.+Utakatifu unaifaa nyumba yako mwenyewe,+ Ee Yehova, kwa wingi wa siku.+