Zaburi 112:1-10

112  Msifuni Yah!+ א [ʼAʹleph]  Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+ ב [Behth]Ambaye amependezwa+ sana na amri zake.+ ג [Giʹmel]   Uzao wake utakuwa wenye nguvu duniani.+ ד [Daʹleth]Nacho kizazi cha wanyoofu, kitabarikiwa.+ ה [Heʼ]   Vitu vyenye thamani na utajiri vimo nyumbani mwake;+ ו [Waw]Nao uadilifu wake unasimama milele.+ ז [Zaʹyin]   Ameangaza katika giza kama nuru kwa walio wanyoofu.+ ח [Chehth]Yeye ni mwenye neema na mwenye rehema na mwadilifu.+ ט [Tehth]   Mtu mwenye neema+ na anayekopesha+ ni mwema. י [Yohdh]Yeye hutegemeza mambo yake kwa haki.+ כ [Kaph]   Kwa kuwa hatatikiswa kamwe.+ ל [Laʹmedh]Mwadilifu atakuwa kumbukumbu mpaka wakati usio na kipimo.+ מ [Mem]   Hataogopa hata habari mbaya.+ נ [Nun]Moyo wake ni imara,+ umefanywa umtegemee Yehova.+ ס [Saʹmekh]   Moyo wake hauwezi kutikiswa;+ hataogopa,+ע [ʽAʹyin]Mpaka awatazame wapinzani wake.+ פ [Peʼ]   Amegawa kwa wingi; amewapa maskini.+ צ [Tsa·dhehʹ]Uadilifu wake unasimama milele.+ ק [Qohph]Pembe yake mwenyewe itainuliwa kwa utukufu.+ ר [Rehsh] 10  Mwovu ataona na hakika atakasirika.+ ש [Shin]Atasaga meno yake na kuyeyuka.+ ת [Taw]Tamaa ya waovu itaangamia.+

Maelezo ya Chini