Zaburi 112:1-10
112 Msifuni Yah!+
א [ʼAʹleph] Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+
ב [Behth]Ambaye amependezwa+ sana na amri zake.+
ג [Giʹmel]
2 Uzao wake utakuwa wenye nguvu duniani.+
ד [Daʹleth]Nacho kizazi cha wanyoofu, kitabarikiwa.+
ה [Heʼ]
3 Vitu vyenye thamani na utajiri vimo nyumbani mwake;+
ו [Waw]Nao uadilifu wake unasimama milele.+
ז [Zaʹyin]
4 Ameangaza katika giza kama nuru kwa walio wanyoofu.+
ח [Chehth]Yeye ni mwenye neema na mwenye rehema na mwadilifu.+
ט [Tehth]
5 Mtu mwenye neema+ na anayekopesha+ ni mwema.
י [Yohdh]Yeye hutegemeza mambo yake kwa haki.+
כ [Kaph]
6 Kwa kuwa hatatikiswa kamwe.+
ל [Laʹmedh]Mwadilifu atakuwa kumbukumbu mpaka wakati usio na kipimo.+
מ [Mem]
7 Hataogopa hata habari mbaya.+
נ [Nun]Moyo wake ni imara,+ umefanywa umtegemee Yehova.+
ס [Saʹmekh]
8 Moyo wake hauwezi kutikiswa;+ hataogopa,+ע [ʽAʹyin]Mpaka awatazame wapinzani wake.+
פ [Peʼ]
9 Amegawa kwa wingi; amewapa maskini.+
צ [Tsa·dhehʹ]Uadilifu wake unasimama milele.+
ק [Qohph]Pembe yake mwenyewe itainuliwa kwa utukufu.+
ר [Rehsh]
10 Mwovu ataona na hakika atakasirika.+
ש [Shin]Atasaga meno yake na kuyeyuka.+
ת [Taw]Tamaa ya waovu itaangamia.+