Zaburi 51:1-19

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Nathani nabii alipoingia kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+ 51  Ee Mungu, unionyeshe kibali kulingana na fadhili zako zenye upendo.+Ufutilie mbali makosa yangu kulingana na wingi wa rehema zako.+   Unioshe kabisa kutokana na kosa langu,+Na kunitakasa kutokana na dhambi yangu.+   Kwa maana mimi mwenyewe nayajua makosa yangu,+Na dhambi yangu iko mbele yangu daima.+   Dhidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda dhambi,+Nami nimefanya lililo baya machoni pako,+Ili uwe mwadilifu unapoongea,+Ili usiwe na lawama unapohukumu.+   Tazama! Nilizaliwa kwa maumivu nikiwa na kosa,+Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.+   Tazama! Umependezwa na ukweli wenyewe katika sehemu za ndani;+Na katika mtu wa sirini unijulishe hekima tupu.+   Unitakase kwa hisopo kutokana na dhambi, ili nipate kuwa safi;+Unioshe, ili nipate kuwa mweupe kuliko theluji.+   Unifanye nisikie kufurahi na kushangilia,+Ili mifupa uliyoiponda ipate kuwa na shangwe.+   Ufiche uso wako kutoka kwa dhambi zangu,+Na ufutilie mbali makosa yangu yote.+ 10  Uumbe moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+Na kuweka ndani yangu roho mpya, iliyo imara.+ 11  Usinitupilie mbali na uso wako;+Wala usiniondolee roho yako takatifu.+ 12  Unirudishie shangwe ya wokovu wako,+Nawe unitegemeze kwa roho ya kupenda.+ 13  Nitawafundisha wakosaji njia zako,+Ili watenda-dhambi wageuke na kurudi kwako kabisa.+ 14  Unikomboe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+Ili ulimi wangu upate kutangaza uadilifu wako kwa shangwe.+ 15  Ee Yehova, na uifungue hii midomo yangu,+Ili kinywa changu mwenyewe kipate kutangaza sifa yako.+ 16  Kwa maana hupendezwi na dhabihu—kama sivyo ningeitoa;+Hupendezwi na toleo zima la kuteketezwa.+ 17  Dhabihu kwa Mungu ni roho iliyovunjika;+Moyo uliovunjika na kupondwa, Ee Mungu, hutaudharau.+ 18  Kwa nia yako njema utendee Sayuni vema;+Na ujenge kuta za Yerusalemu.+ 19  Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,+Na dhabihu za kuteketezwa na toleo zima;+Ndipo ng’ombe-dume watakapotolewa katika madhabahu yako mwenyewe.+

Maelezo ya Chini