Zaburi 51:1-19
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Nathani nabii alipoingia kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+
51 Ee Mungu, unionyeshe kibali kulingana na fadhili zako zenye upendo.+Ufutilie mbali makosa yangu kulingana na wingi wa rehema zako.+
2 Unioshe kabisa kutokana na kosa langu,+Na kunitakasa kutokana na dhambi yangu.+
3 Kwa maana mimi mwenyewe nayajua makosa yangu,+Na dhambi yangu iko mbele yangu daima.+
4 Dhidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda dhambi,+Nami nimefanya lililo baya machoni pako,+Ili uwe mwadilifu unapoongea,+Ili usiwe na lawama unapohukumu.+
5 Tazama! Nilizaliwa kwa maumivu nikiwa na kosa,+Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.+
6 Tazama! Umependezwa na ukweli wenyewe katika sehemu za ndani;+Na katika mtu wa sirini unijulishe hekima tupu.+
7 Unitakase kwa hisopo kutokana na dhambi, ili nipate kuwa safi;+Unioshe, ili nipate kuwa mweupe kuliko theluji.+
8 Unifanye nisikie kufurahi na kushangilia,+Ili mifupa uliyoiponda ipate kuwa na shangwe.+
9 Ufiche uso wako kutoka kwa dhambi zangu,+Na ufutilie mbali makosa yangu yote.+
10 Uumbe moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+Na kuweka ndani yangu roho mpya, iliyo imara.+
11 Usinitupilie mbali na uso wako;+Wala usiniondolee roho yako takatifu.+
12 Unirudishie shangwe ya wokovu wako,+Nawe unitegemeze kwa roho ya kupenda.+
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,+Ili watenda-dhambi wageuke na kurudi kwako kabisa.+
14 Unikomboe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+Ili ulimi wangu upate kutangaza uadilifu wako kwa shangwe.+
15 Ee Yehova, na uifungue hii midomo yangu,+Ili kinywa changu mwenyewe kipate kutangaza sifa yako.+
16 Kwa maana hupendezwi na dhabihu—kama sivyo ningeitoa;+Hupendezwi na toleo zima la kuteketezwa.+
17 Dhabihu kwa Mungu ni roho iliyovunjika;+Moyo uliovunjika na kupondwa, Ee Mungu, hutaudharau.+
18 Kwa nia yako njema utendee Sayuni vema;+Na ujenge kuta za Yerusalemu.+
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,+Na dhabihu za kuteketezwa na toleo zima;+Ndipo ng’ombe-dume watakapotolewa katika madhabahu yako mwenyewe.+