Zaburi 2:1-12

2  Kwa nini mataifa yamekuwa na fujo+Na vikundi vya mataifa vimeendelea kusema jambo la upuuzi?+   Wafalme wa dunia wanachukua msimamo wao+Nao maofisa wakuu wamejikusanya pamoja kama mtu mmoja+Dhidi ya Yehova+ na dhidi ya mtiwa-mafuta wake,+   Wakisema: “Na tuzikate pingu zao+Na kuzitupa kamba zao mbali nasi!”+   Yule anayeketi mbinguni+ atacheka;Yehova mwenyewe atawadharau.+   Wakati huo atasema nao katika hasira yake+Na katika ghadhabu yake atawafadhaisha,+   Na kusema: “Mimi, naam, mimi nimemweka mfalme wangu+Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”+   Acheni nirejezee agizo la Yehova;Yeye ameniambia: “Wewe ni mwanangu;+Mimi, leo, nimekuwa baba yako.+   Niombe,+ ili nikupe mataifa yawe urithi wako+Na miisho ya dunia iwe miliki yako mwenyewe.+   Utawavunja kwa fimbo ya chuma ya enzi,+Utawavunja vipande-vipande, kama chombo cha mfinyanzi.”+ 10  Na sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;Kubalini kurekebishwa, enyi waamuzi wa dunia.+ 11  Mtumikieni Yehova kwa woga+Na mshangilie kwa kutetemeka.+ 12  Mbusuni mwana,+ ili Yeye asikasirikeNanyi msiangamizwe kutoka njiani,+ Kwa maana hasira yake huwaka kwa urahisi.+Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia.+

Maelezo ya Chini