Zaburi 25:1-22

Ya Daudi. א [ʼAʹleph] 25  Kwako wewe, Ee Yehova, naiinua nafsi yangu.+ ב [Behth]   Ee Mungu wangu, nimekutegemea wewe;+Ee nisione aibu.Adui zangu na wasishangilie juu yangu.+ ג [Giʹmel]   Pia, hakuna yeyote kati ya wale wanaokutumainia atakayeona aibu.+Wale wanaotenda kwa hila bila kupata mafanikio wataona aibu.+ ד [Daʹleth]   Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+Nifundishe mapito yako mwenyewe.+ ה [Heʼ]   Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.+ ו [Waw]Nimekutumainia mchana kutwa.+ ז [Zaʹyin]   Ukumbuke rehema zako,+ Ee Yehova, na fadhili zako zenye upendo,+Kwa maana ni za tangu wakati usio na kipimo.+ ח [Chehth]   Usizikumbuke dhambi za ujana wangu na maasi yangu.+Unikumbuke kulingana na fadhili zako zenye upendo,+Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+ ט [Tehth]   Yehova ni mwema na mnyoofu.+Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda-dhambi katika ile njia.+ י [Yohdh]   Atawafanya wapole watembee katika uamuzi wake wa hukumu,+Naye atawafundisha wapole njia yake.+ כ [Kaph] 10  Mapito yote ya Yehova ni fadhili zenye upendo na ukweliKwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+ ל [Laʹmedh] 11  Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+Usamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.+ מ [Mem] 12  Sasa, ni nani anayemwogopa Yehova?+Atamfundisha katika njia ambayo yeye ataichagua.+ נ [Nun] 13  Nafsi yake itakaa katika wema,+Na uzao wake mwenyewe utaimiliki dunia.+ ס [Saʹmekh] 14  Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+Pia agano lake, ili kuwafanya walijue.+ ע [ʽAʹyin] 15  Macho yangu yanamwelekea Yehova daima,+Kwa maana yeye ndiye huitoa miguu yangu katika wavu.+ פ [Peʼ] 16  Unielekezee uso wako, na unionyeshe kibali;+Kwa maana mimi niko peke yangu nami ni mwenye kuteseka.+ צ [Tsa·dhehʹ] 17  Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+Uniondoe katika mikazo iliyo juu yangu.+ ר [Rehsh] 18  Uone mateso yangu na taabu yangu,+Na unisamehe dhambi zangu zote.+ 19  Uone jinsi adui zangu wamekuwa wengi,+Nao wamenichukia kwa chuki yenye jeuri.+ ש [Shin] 20  Uilinde nafsi yangu na kunikomboa.+Nisione aibu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+ ת [Taw] 21  Utimilifu na unyoofu na zinilinde,+Kwa maana nimekutumainia wewe.+ 22  Ee Mungu, mkomboe Israeli kutoka katika taabu zake zote.+

Maelezo ya Chini