Zaburi 25:1-22
Ya Daudi.
א [ʼAʹleph]
25 Kwako wewe, Ee Yehova, naiinua nafsi yangu.+
ב [Behth]
2 Ee Mungu wangu, nimekutegemea wewe;+Ee nisione aibu.Adui zangu na wasishangilie juu yangu.+
ג [Giʹmel]
3 Pia, hakuna yeyote kati ya wale wanaokutumainia atakayeona aibu.+Wale wanaotenda kwa hila bila kupata mafanikio wataona aibu.+
ד [Daʹleth]
4 Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+Nifundishe mapito yako mwenyewe.+
ה [Heʼ]
5 Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.+
ו [Waw]Nimekutumainia mchana kutwa.+
ז [Zaʹyin]
6 Ukumbuke rehema zako,+ Ee Yehova, na fadhili zako zenye upendo,+Kwa maana ni za tangu wakati usio na kipimo.+
ח [Chehth]
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu na maasi yangu.+Unikumbuke kulingana na fadhili zako zenye upendo,+Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+
ט [Tehth]
8 Yehova ni mwema na mnyoofu.+Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda-dhambi katika ile njia.+
י [Yohdh]
9 Atawafanya wapole watembee katika uamuzi wake wa hukumu,+Naye atawafundisha wapole njia yake.+
כ [Kaph]
10 Mapito yote ya Yehova ni fadhili zenye upendo na ukweliKwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+
ל [Laʹmedh]
11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+Usamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.+
מ [Mem]
12 Sasa, ni nani anayemwogopa Yehova?+Atamfundisha katika njia ambayo yeye ataichagua.+
נ [Nun]
13 Nafsi yake itakaa katika wema,+Na uzao wake mwenyewe utaimiliki dunia.+
ס [Saʹmekh]
14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+Pia agano lake, ili kuwafanya walijue.+
ע [ʽAʹyin]
15 Macho yangu yanamwelekea Yehova daima,+Kwa maana yeye ndiye huitoa miguu yangu katika wavu.+
פ [Peʼ]
16 Unielekezee uso wako, na unionyeshe kibali;+Kwa maana mimi niko peke yangu nami ni mwenye kuteseka.+
צ [Tsa·dhehʹ]
17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+Uniondoe katika mikazo iliyo juu yangu.+
ר [Rehsh]
18 Uone mateso yangu na taabu yangu,+Na unisamehe dhambi zangu zote.+
19 Uone jinsi adui zangu wamekuwa wengi,+Nao wamenichukia kwa chuki yenye jeuri.+
ש [Shin]
20 Uilinde nafsi yangu na kunikomboa.+Nisione aibu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
ת [Taw]
21 Utimilifu na unyoofu na zinilinde,+Kwa maana nimekutumainia wewe.+
22 Ee Mungu, mkomboe Israeli kutoka katika taabu zake zote.+