Zaburi 42:1-11
Kwa kiongozi. Maskili kwa ajili ya wana wa Kora.+
42 Kama vile paa ambaye hutamani vijito vya maji,Ndivyo nafsi yangu inavyokutamani wewe, Ee Mungu.+
2 Kwa kweli nafsi yangu ina kiu kwa ajili ya Mungu,+ kwa ajili ya Mungu aliye hai.+Ni wakati gani nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?+
3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku,+Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+
4 Nitakumbuka mambo haya, nami nitaimimina nafsi yangu iliyo ndani yangu.+Kwa maana nilikuwa nikipita pamoja na watu wengi,Nilikuwa nikitembea polepole mbele yao kwenda kwenye nyumba ya Mungu,+Kwa sauti ya vigelegele vya shangwe na shukrani,+Ya umati unaofanya sherehe.+
5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu.+
6 Ee Mungu wangu, nafsi yangu mwenyewe imekata tamaa ndani yangu.+Ndiyo sababu ninakukumbuka,+Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,+Kutoka katika ule mlima mdogo.+
7 Kilindi cha maji kinaita kilindi cha majiKwa sauti ya mabubujiko yako ya maji.Mashuu yako yote na mawimbi yako+—Yamepita juu yangu.+
8 Wakati wa mchana Yehova ataamuru fadhili zake zenye upendo,+Na wakati wa usiku wimbo wake utakuwa nami;+Kutakuwako sala kwa Mungu wa uhai wangu.+
9 Nitamwambia Mungu mwamba wangu:+“Kwa nini umenisahau?+Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?”+
10 Wale wanaonionyesha uadui wamenishutumu kwa mauaji dhidi ya mifupa yangu,+Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+
11 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+