Zaburi 42:1-11

Kwa kiongozi. Maskili kwa ajili ya wana wa Kora.+ 42  Kama vile paa ambaye hutamani vijito vya maji,Ndivyo nafsi yangu inavyokutamani wewe, Ee Mungu.+   Kwa kweli nafsi yangu ina kiu kwa ajili ya Mungu,+ kwa ajili ya Mungu aliye hai.+Ni wakati gani nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?+   Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku,+Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+   Nitakumbuka mambo haya, nami nitaimimina nafsi yangu iliyo ndani yangu.+Kwa maana nilikuwa nikipita pamoja na watu wengi,Nilikuwa nikitembea polepole mbele yao kwenda kwenye nyumba ya Mungu,+Kwa sauti ya vigelegele vya shangwe na shukrani,+Ya umati unaofanya sherehe.+   Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu.+   Ee Mungu wangu, nafsi yangu mwenyewe imekata tamaa ndani yangu.+Ndiyo sababu ninakukumbuka,+Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,+Kutoka katika ule mlima mdogo.+   Kilindi cha maji kinaita kilindi cha majiKwa sauti ya mabubujiko yako ya maji.Mashuu yako yote na mawimbi yako+Yamepita juu yangu.+   Wakati wa mchana Yehova ataamuru fadhili zake zenye upendo,+Na wakati wa usiku wimbo wake utakuwa nami;+Kutakuwako sala kwa Mungu wa uhai wangu.+   Nitamwambia Mungu mwamba wangu:+“Kwa nini umenisahau?+Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?”+ 10  Wale wanaonionyesha uadui wamenishutumu kwa mauaji dhidi ya mifupa yangu,+Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+ 11  Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu na kuwa ndiye Mungu wangu.+

Maelezo ya Chini