Zaburi 84:1-12
Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya wana wa Kora. Muziki.
84 Jinsi ilivyo nzuri maskani yako kuu,+Ee Yehova wa majeshi!+
2 Nafsi yangu imetamani sana na pia imedhoofika kwa kutamani nyua za Yehova.+Moyo wangu mwenyewe na mwili wangu wenyewe humpigia Mungu aliye hai vigelegele kwa shangwe.+
3 Hata ndege amepata nyumba,Na mbayuwayu amepata kiota chake,Ambapo ameweka vifaranga vyake—Madhabahu yako kuu, Ee Yehova wa majeshi, Mfalme wangu na Mungu wangu!
4 Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+Bado wanaendelea kukusifu.+ Sela.
5 Wanadamu wenye furaha ni wale ambao nguvu zao ziko kwako,+Ambao njia kuu zimo moyoni mwao.+
6 Wakipita katika nchi tambarare ya chini ya mibaka,+Wanaigeuza kuwa bubujiko;Naam, mfundishaji+ anajivika baraka.
7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu hata nguvu;+Kila mmoja huonekana mbele za Mungu katika Sayuni.+
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, usikie sala yangu;+Utege sikio, Ee Mungu wa Yakobo.+ Sela.
9 Ee ngao yetu, ona, Ee Mungu,+Na uutazame uso wa mtiwa-mafuta wako.+
10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko.+Nimechagua kusimama mlangoni pa nyumba ya Mungu wangu+Badala ya kuzunguka katika mahema ya uovu.+
11 Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+Yeye hutoa kibali na utukufu.+Yehova mwenyewe hatawanyima jambo lolote jema wale wanaotembea bila kosa.+
12 Ee Yehova wa majeshi, mtu mwenye furaha ni yule anayekutegemea.+