Zaburi 85:1-13

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki. 85  Ee Yehova, umependezwa na nchi yako;+Umewarudisha wale waliochukuliwa mateka wa Yakobo.+   Umelisamehe kosa la watu wako;+Umeifunika dhambi yao yote.+ Sela.   Umeizuia ghadhabu yako yote;+Umegeuka kutoka kwenye moto wa hasira yako.+   Utukusanye tena, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Na uache kutukasirikia.+   Je, utapandwa na hasira kwa sababu yetu mpaka wakati usio na kipimo?+Je, utarefusha hasira yako kizazi baada ya kizazi?+   Je, hutatufanya hai tena,+Ili watu wako wapate kushangilia ndani yako?+   Ee Yehova, utuonyeshe fadhili zako zenye upendo,+Nawe utupe wokovu wako.+   Nitasikia jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova atasema,+Kwa maana atasema amani kwa watu wake+ na kwa washikamanifu wake,Lakini wasirudi kujitumaini.+   Hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+Ili utukufu ukae katika nchi yetu.+ 10  Nazo fadhili zenye upendo na ukweli, zimekutana;+Uadilifu na amani—zimepigana busu.+ 11  Ukweli utachipuka kutoka duniani,+Nao uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+ 12  Pia, Yehova atatoa yaliyo mema,+Nayo nchi yetu wenyewe itatoa mazao yake.+ 13  Mbele zake uadilifu wenyewe utatembea,+Nao utafanya njia kwa hatua zake.+

Maelezo ya Chini