Zaburi 85:1-13
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.
85 Ee Yehova, umependezwa na nchi yako;+Umewarudisha wale waliochukuliwa mateka wa Yakobo.+
2 Umelisamehe kosa la watu wako;+Umeifunika dhambi yao yote.+ Sela.
3 Umeizuia ghadhabu yako yote;+Umegeuka kutoka kwenye moto wa hasira yako.+
4 Utukusanye tena, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Na uache kutukasirikia.+
5 Je, utapandwa na hasira kwa sababu yetu mpaka wakati usio na kipimo?+Je, utarefusha hasira yako kizazi baada ya kizazi?+
6 Je, hutatufanya hai tena,+Ili watu wako wapate kushangilia ndani yako?+
7 Ee Yehova, utuonyeshe fadhili zako zenye upendo,+Nawe utupe wokovu wako.+
8 Nitasikia jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova atasema,+Kwa maana atasema amani kwa watu wake+ na kwa washikamanifu wake,Lakini wasirudi kujitumaini.+
9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+Ili utukufu ukae katika nchi yetu.+
10 Nazo fadhili zenye upendo na ukweli, zimekutana;+Uadilifu na amani—zimepigana busu.+
11 Ukweli utachipuka kutoka duniani,+Nao uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+
12 Pia, Yehova atatoa yaliyo mema,+Nayo nchi yetu wenyewe itatoa mazao yake.+
13 Mbele zake uadilifu wenyewe utatembea,+Nao utafanya njia kwa hatua zake.+